Thursday, August 21 2025

Header Ads

TAMTHILIA YA WALANG HANGGAN YAZIDI KUKONGA NYOYO ZA WATAZAMAJI WA STAR TV.

Katerina, Nathan, Johan, Thomas na Daniel

Baada ya baba yake Katerina kufariki ghafla, sasa Thomasi “mwanae” anajimilikisha kampuni ya baba yake kinyume na mirathi ya baba yake, huku akimfanyia unyama Daniel.

Thomas anagundua kuwa Daniel na mdogo wake Katerina wanauhusiano wa kimapenzi, hivyo anatekwa na wivu na kuamua kumsingizia Daniel kuwa ameiba pesa. Thomas anaamua kumpa adhabu ya kumfunga  kamba mikono  na kumburuza katika shamba la baba yake.

Lakini wakati Thomas akimfanyia unyama huo Daniel, Emily anaye sadikika kuwa huenda akawa ni mama yake alishuhudia kwa mbali mkasa huo, kitu kilicho mkwaza sana na kumuamulu  mfanyakazi wake kumfuatilia Thomas na kubaini chanzo.

Thomas naamua kuchoma sehemu ya nyumba na kumsingizia Daniel, ili kwamba iwe rahisi kumuhamisha Katerina pale ili akae mbali na Daniel. Thomas anampigia sana debe Nathan awe mpenzi wa mdogo wake Katerina, sababu iliyomfanya amuhamishie Katerina kwao Nathan ili baadae familia ya Nathan iweze kumsaidia kifedha.

Emily anazidi kumtumia Johane binti yake Marco ili kupata upenyo mzuri wa kulipiza kisasi katika familia hiyo. Emily ambaye sasa maisha yake ni mazuri kifedha anaingiwa na huruma mara kwa mara akikumbuka kitendo cha Thomas kumburuza Daniel na farasi, hivyo sasa anaanza kumfuatilia Daniel kujua mengi japokuwa ameambiwa kuwa Daniel ni mototo wa kambo.

Siri nzito yapangwa kufichuliwa na bibi yake Daniel, huku Emily akijipanga kulipiza kisasi kwa familia ya Marco.

Je nini kitaendelea?  Karibu tena kwa dondoo  nyingine za tamthilia hii hapa hapa.

Leave a Comment

Powered by Blogger.