Wednesday, April 30 2025

Header Ads

PICHA ZA VIVUTIO VYA ASILI VITENGENEZWAVYO NA WANAWAKE MKOANI ARUSHA.

Asili Yetu © All rights reserved

 Wanawake mkoani Arusha wamekuwa mstari wa mbele katika kujikita katika kazi mbali mbali za mikono kama vile kutengeneza vyombo  vya asili ambavyo vimekuwa ni kivutio kikubwa kwa watalii wanaoingia na kutoka mjini Arusha. Hii ni hatua mojawapo kwa akinamama hawa kupiga kwani wanadhihirisha kuwa, kazi nzuri hazitengezwi na wanaume tu bali  ubunifu mzuri wa vyombo vya asili hutengenezwa pia na akinamama ambao ni watalaam wa kutambua rangi zipendwazo na watu wa sasa.

Kazi hizi uzionazo hapa ni juhudi, utaalamuna ubunifu wa hali ya juu ufanywao na akinamama hawa ambao pia ni nguzo katika familia zao. Huu ni utamaduni halisi wa kitanzania ambao ndio unaotufanya tutembee vifua mbele tuwapo katika mataifa mengine duniani.

Eneo hili  lililoko mjini Arusha ni maarufu kwa vitu mbali mbali vya asili ambavyo wageni na wenyeji huja kununua.

Kama unavyoona hapa ni mbele ya eneo maalum la kuuzia vyombo vya asili mjini Arusha.


Hivi ni viatu ambavyo hutengenezwa kwa kutumia matairi ya gari yaliyokwisha kutumika.Viatu hivi ni maarufu kama "kata mbuga" japokuwa vinamajina mengi sana kulingana na sehemu zitumikazo.

Hizi ni picha zilizochorwa kwa mkono, lakini pia kuna viatu vya wazi vya asili ambavyo havipitwi na wakati.Hiatu hivi hutengenezwa kwa ngozi na kutiwa nakshi ya shanga zenye rangi mbali mbali.


Leave a Comment

Powered by Blogger.