WALANG HANGGAN (TAMTHILIA) - EPISODE YA 5&6 DANIEL AUTEKA MOYO WA KATERINA NAKUJIKUTA AKIZAMA KATIKA PENZI ZITO LA KIFICHO.
![]() |
| Daniel, Katerina (kati) na Nathan |
Kwa kifupi sherehe inavurugika na Daniel kuamua kwenda mbali
kidogo na makazi yao, sehemu nzuri za miinuko na nyasi za kijani ambapo kando
kando yake kunaonekana ufukwe wa bahari. Lakini Daniel akiwa huko na mwenye
majonzi, mara Katerina anawasiri katika eneo hilo na kumwagia Daniela lawama
nzito kwa kumwalibia sherehe yake, kwani alitegemea mengi kutokea.
Daniela namuomba msamaha lakini Katerina na anazidi kumlaumu
Daniela na kusema “umeniharibia sherehe yangu kwa ugomvi, kwani nimekosa vitu
vingi vya msingi ambavyo ningevipata” Daniel akiwa bado anashangaa, mara
Katerina akagundua kuwa Daniel hakuwa na ile pete inayompagawisha siku zote,
hivyo anaamua kumuuliza kama alimpatia msichana mwingine.
Daniel anatabasam na kutoa kitu mfukoni na kukifunua…… woow!
Ilikuwa ni ile pete inayompagawisha Katerina siku zote! Katerina anaamuuliza
Daniel…. Ni nini hicho? Daniela anatoa ile pete na kumvisha…. Mmmh! Tayari
wanakula kiapo kuwa wapenzi katika maisha yao yote…. Ila swala hili bado
Katerina anapendekeza liwe siri kwa baba yake mpaka atakapomaliza shule.
Bibi yake Daniel anasanukia mchongo huo na kuamua kuwauliza
wakiwa wote wawili, Daniel anaamua kuto mficha bibi yake kuhusu mahusiano yake
na Katerina. Bibi yao anawasihi kutofanya mambo ya kikubwa mpaka hapo muda
utakapofika……
Kumbuka Tamthilia hii ilianzwa na Marco Montenegro na Emily
ambapo Emily aliwekwa jela na mama yake Marco, huku Emily pia akizaa mtoto na
kudaiwa kufariki mara tu baada ya kuzaliwa.
Sasa Emily alishatoka Jela na ni tajiri ambaye amepanga
kulipiza kisasi kwa familia ya Marco Montenegro. Emily tayari anamtuma mfuasi
wake mmoja akiwa kama mfanyakazi katika familia ya Marco ili apeleleze mpango
mzima, kwani familia hiyo haikuwepo huko muda mrefu.
Baba yake Katerina anapata safari ya kwenda mji mwingine na
kumuagiza pia Daniel kwenda mji wa Manila kumfuatilia Thomas ambaye ni kaka
yake Katerina, ili kujua maendeleo ya kampuni aliyodai kuwa anaanzisha.
Kabla Daniel hajaenda Manila, Nathan Montenegro ambaye
alikuwa ni rafiki wa karibu wa Katerina wakati wa utoto ambaye kwa kipindi
kirefu hawakuwa wanaonana, alifika ghafla nyumbani kwa kina Katerina na
kumuomba waende wote kwa wazazi wake ili kuwasabahi.
Katerina akiwa nyumbani kwa akina Nathan, huku Daniel
alianza kumtafuta ikaambiwa kuwa ameondoka na Nathan.
Daniel anaamua kwenda hadi kwa akina Nathan na kuzuiliwa
kuingia kwani kulikuwa na walinzi. Kule ndani Nathan anamzuia Katerina kuondoka
na kudai anamletea kinywaji. Katerina anaamua kuzunguka zunguka ndani lakini
hakuona mtu yeyote, anamua kwenda kibarazani mara anakutana na Daniel ambaye
aliamua kuruka ukuta na kuingia huko ndani ya fensi.
Wakiwa bado wamesimama, mara mbwa mkubwa anatokeza na
kuwanza kuwafukuza, ila kwa ujasili Daniel anamwambia Katerina “usikimbie
jikaze usimame hivo hivo” lakini uzalendo unamshinda Katerina na kuanza
kukimbia. Mbwa inamuuma mguu baada ya kuwa ameanguka.
Walinzi wanambeba na kumpeleka ndani, huku Daniel akikatazwa
kuingia huku akionyeshewa bastola. Marco Montenegro anampigia simu baba yake
Katerina na kumuomba akae kwake ili apone vizuri. Marco anaamua kumpa rifti
Daniel kwenda mji wa Manila ambako baba yake Katerina alimuagiza. Lakini huko
nyuma fisi anakabidhiwa bucha, yana Katerina anabaki na Nathan….. Je nini
kitatokea katika mahusiano ya Daniel na Katerina?
Huko mjini nako Marco Montenegro anamuona Emily kwa macho
yake yani live, Je nini kitatokea?
Je nini kitaendelea? Karibu tena
kwa dondoo nyingine za tamthilia hii
hapa hapa.

No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA