MASKINI “DANIEL CRUZ” AZIDI KUFANYIWA UNYAMA NDANI YA TAMTHILIA YA “WALANG HANGGAN”.
Baada ya Thomas kumfanyia unyama wa kumburuza Daniel Cruz na
farasi, hakuridhika kwani sasa Thomas aungana na rafiki zake na kumpa kichapo
kibaya japokuwa haikuwa rahisi kwao kwani kama kawaida Daniel Cruz aliwatembezea
kichapo, japokuwa wakati huu walimzidi na kumchoma kisu ubavuni na kumtupa
mtoni.
Kumbuka chanzo cha Daniel Cruz kupata matatizo yote hayo ni
mdogo wake Thomas anayeitwa Katerina ambaye amezama katika penzi la Daniel
Cruz. Kwasababu Katerina hakuwepo nyumbani kwa muda mrefu akiwa nyumbani kwa
akina Nathan Montenegro sasa aamua kurejea nyumbani kwao ili apate muda mzuri
wa kuwa na Daniel Cruz.
Akimuelezea Nanni (bibi yake Daniel Cruz) jinsi Nathan
anavyokazana kumtongoza na kumuahidi kumuoa, mara Daniel Cruz alifika kimia
kimia na kuyasikia maneno hayo, kitu kilichomsababisha kumwaga machozi na
kuamua kwenda porini ambako ndiko Thomas na rafiki zake walimchoma kisu na
kumtupa mtoni.
Katerina anashikwa na machale kwa kutomuona Daniel, akiwa na
hofu huku akimwaga machozi kama mvua ya elinino ya miaka ya 90 naa, juhudi hizo
zinagonga mwamba na kuambulia kwenda kutoa taarifa polisi. Kumbe mpango mzima
wa mauwaji ya Daniel Cruz yalipangwa na Nathan Marco Montenegro ambae amekuwa
akimgombea Kateria.
Mungu mkubwa Daniel Cruz hakufariki wakati ule alipotupwa
mtoni huku akiwa amechomwa kisu ubavuni, alijikongoja hadi kando kando ya bara
bara na kupoteza fahamu. Emily adui mkubwa wa familia ya Marco Montenegro
wakiwa katika mishe mishe yao wanamkuta Danie Cruz akiwa katika hali mbaya.
Emily anawaamrisha watu wake wampakie garini na na kumuwahisha hospitali.
Mungu saidia Daniel Cruz asilimia kubwa anapona akiwa
nyumbani kwa Emily. Daniel anadai aondoke na kurudi kwa Thomas, lakini Emiliy
anamshauri asirudi mapema bali aandamane nae kwenda katika mji mwingine ambako
huko atamtajirisha ili aweze kulipiza kisasi kwa Montenegro na Thomas.
Emily anamuomba Daniel Cruz abadili jina na awe kama kijana
wake mkubwa ili Montenegro wasije kumfatilia kwa urahisi. Daniel Cruz bado
hajaridhia uamuzi huo, lakini kunakitu kinatokea kinachomfanya akubaliana na
wazo la Emily.
Je nini kitaendelea? Karibu tena
kwa dondoo nyingine za tamthilia hii
hapa hapa.

No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA