HATIMAE MSANII WA MAIGIZO "MATUMAINI ALIYEKUWA AKIUGUA HUKO NCHINI ZAMBIA AREJESHWA TANZANIA.
Matumaini (kulia) akiwa na Bi. Mwenda (wa pili kushoto) na
anayefuata (kushoto) ni msanii mwenzake Kiwewe wakisubiri gari la kumpeleka
hospitali.
Matumaini akiwa amebebwa mgongoni na msanii mwenzake, Mariam Athuman ‘Kalunde’ akimpeleka kwenye gari.
MSANII wa vichekesho ambaye alikuwa nchini Msumbiji, Tumaini
Mwakibibi ‘Matumaini’ jana alipokelewa na wasanii wenzake kibao baada ya kutua
katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar akiwa hoi
kutokana na kusumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.
Matumaini alitua uwanjani hapo jana majira ya saa 9:30
alasiri ambapo kutokana na hali yake kuwa mbaya wasanii walimbeba mgongoni na
kumfikisha kwenye gari ambapo walimpeleka moja kwa moja hospitali ya Amana
alikolazwa mpaka sasa akiendelea kupatiwa matibabu.
Matumaini akiwa amebebwa mgongoni na msanii mwenzake, Mariam Athuman ‘Kalunde’ akimpeleka kwenye gari.
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini (TAFF), Simon
Mwakifwamba akizungumza na wasanii maeneo ya Amana wakati Matumaini akiwa kwa
daktari.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS



No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA