Header Ads

Breaking News
recent

WENYE VIRUSI VYA UKIMWI WATAKIWA KUJIANDIKISHA ILI WASAIDIWE.


WAKAZI wa Mtaa wa Kipunguni Manispaa ya Ilala, ambao wanaishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) wametakiwa kwenda kujiandikisha katika ofisi za serikali za mtaa huo kwa ajili ya kusaidiwa huduma mbalimbali.

Akizungumza Dar es Salaam jana wakati wa mkutano wa hadhara, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kipunguni, Praxeda Mkandara, alisema kwa kawaida huwa kuna fungu la Sh300,000 linalotolewa na manispaa kwa ajili ya kusaidia waathirika wa Ukimwi.

Alisema fungu hilo hutolewa kila baada ya miezi sita na kwamba ili mtu asaidiwe anatakiwa kwenda na uthibitisho wa vyeti ambavyo vinaonyesha kuwa anaishi na Viruisi vya Ukimwi (VVU).

Hata hivyo baadhi ya wakazi wa mtaa huo walitilia shaka suala hilo kwa madai kuwa kutokana na hali ngumu ya maisha watu wengine wanaweza kugushi vyeti ili waonekane wameathirika kwa lengo la kupatiwa misaada.
“Watu wengi wamepigika na maisha ukisema mtu aje na cheti wengine wanaweza kutumia nafasi hiyo kugushi vyeti ili wapate misaada,”alisema mmoja wa wakazi hao Mbaga Zacharia.

Mwenyekiti huyo alisema wanazo taratibu mbalimbali na kwamba huwa hawatoi misaada hiyo hadi wajiridhishe ili misaada iwafikie walengwa husika.
Pia aliwataka wakazi ambao hawajui kusoma na kuandika wajitokeze kwenye madarasa ya elimu ya watu wazima ili waweze kupatiwa elimu hiyo.

Katika hatua nyingine, diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa, akizungumza kwenye mkutano huo, aliwataka watu wanaotaka zabuni za kufanya usafi kwenye mitaa mbalimbali ya kata hiyo wajiunge kwenye vikundi kama vya wajane na vijana.

Alisema lengo lao ni kuhakikisha fedha hizo zinarudi kwa wananchi wenyewe ili waweze kujipatia kipato.Diwani huyo pia alisema hivi sasa waameanza ukarabati wa makaravati baada ya kupata fedha za mfuko wa jimbo ambazo ni Sh7.5 milioni.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.