KOCHA WA HARAMBEE STARS YA KENYA, AJIHUZULU.
Aliyekuwa kocha wa Kenya
Kocha wa
Harambee Stars Henri Michel amejiuzulu miezi minne tu baada ya kusaini
mkataba na shirikisho la mchezo wa soka nchini Kenya FKF.
Michel hulipwa shillingi milioni nne na manaibu wake wawili nao hupokea mshahara wa milioni moja unusu.
Kwa mujibu wa barua kutoka kwa Ubalozi wa Ufaransa mjini Nairobi kocha huyo anarejea nyumbani hii leo.
Hata hivyo barua hiyo inaashirikia kuwa kocha huyo alijiuzulu tarehe kumi mwezi huu lakini tangazo hilo limetolewa leo tarehe 17 Desemba.
Michel alikataa kuongoza Harambee Stars wakati wa michuano ya kuwania kombe la mataifa bingwa kanda ya Afrika Mashariki na Kati CECAFA, akiitaja mashindano hayo kama mashindano yasiyokuwa na maana yoyote.
Aliyekuwa kocha wa Kenya Henri Mitchel
Awali rais wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Kenya Sam Nyamweya alikariri kuwa kocha huyo alikuwa na jukumu la kuandaa Harambee Stars kwa michuano ya kufuzu kwa kombe la dunia mwaka wa 2014.
Source: BBC
No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA