Header Ads

Breaking News
recent

CHADEMA MKOA WA ARUSHA YAPATA VYOMBO VYA MUZIKI KWA AJILI YA MIKUTANO


Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiwa anawashukuru wanachini na wadau ambao walifanikisha ununuzi wa vyombo vya chama mkoa wa arusha  wakati walipokuwa wameudhuria kwenye eventya M4C-JOIN THE CHAIN iliyofanyika katika ukumbi wa hotel ya snowcrest jijini Arusha.


Lema akiwa na baadhi ya wanachama ambao ni wadau wakubwa wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema ambapo alisema kuwa wadau hawa wanatarajia kuingia katika majimbo mbalimbali hapa nchini kwa ajili ya kuwaletea watanzania ukombozi.


Katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema mkoa wa arusha Amani Golugwa.

Kwaupande wake Katibu wa mkoa Chadema Amani Golugwa aliwashukuru sana wadau wote ambao wameuthuria na kushiriki katika shughuli hii ya kuchangia vyombo pamoja na kuchangia gari lakubebea vyombo na alibainisha kuwa wakati huu ni wa mabadiliko wanafanya kazi kwakusonga mbele na hawatakubali kurudishwa nyumba huku akibainishakuwa wakati huu sio wakuulizana nani mwizi bali ni wakati wa kukamata mwizi nakufanya kazi tu

Alisema kuwa swala la mabadililiko ni mpango wa mungu hivyo hakuna mtu yeyote ambaye anawezakuzuia mipango wa mungu aku akisema kuwa wanajua itachukuwa muda lakini lazima mabadiliko yatatokea tu.
Aliseongeza kuwa kwakipindi hichi wameamua kuanzisha M4C JOIN THE CHAIN  hiii ikiwa ni njia ya kuleta mabaidiliko huku akisema kuwa wanataka wanyakuwe majimbo yote ya mkoa wa Arusha
"unajua tunataka tunyakuwe majimbo yote ya mkoa wa arusha nakwanza kabla ya kuyachukuwa tunataka tuanze kuwaonyesha wananchi katika baadhi ya halmashauri tulizo zichukuwa ambapo alisema kuwa wao kama chadema mkoa wa Arusha wanamiliki halmashauri mbili ambayo ni halmashauri ya meru pamoja na karatu ambapo alisema hizi ndo anataka ziwe za mfano katika kuleta maendeleo.

Alifafanua kuwa vyombo vya mziki vilivyonunuliwa (pa system)viligharimu kiasi chashilingi  milioni 14 na laki sita  ,huku kiasi cha shilingi milini 27 zikiwa ni ahadi kwaajili ya gari na keshi ikiwa ni shilingi milioni moja.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.