Header Ads

Breaking News
recent

MSANII LORD EYES: WAKILI WAKE ATOA UFAFANUZI KWA WAANDISHI WA HABARI KUFUATIWA TUHUMA ZINAZOMKABILI LORD EYEZ.


Msanii Lord Eyes na mwanasheria wake Peter Kibatala wakiwa Double View ambapo walizungumza na waandishi wa habari.

Msemaji wa kundi la WEUSI Nikki wa Pili,Mwanasheria,Lord Eyes na G Warawara.
Wakili wa Lord Eyes leo ametoa ufanunuzi kuhusu tukio lililotokea la msanii huyo kuhusishwa na wizi wa vifaa vya kwenye gari.Wakili huyo alisema kua dhumuni la kuwaita waandishi wa habari leo ni kutaka Jamii itoe nafasi kwa vyombo vya sheria kutoa majibu juu ya tuhuma hizo baada ya hapo ndo waanze kuongea.

Sahivi kinachoendelea ni habari ambazo watu hawana uhakika nazo.Wakili huyo alisema kuwa Lord Eyes hana hatia hadi pale vyombo vya sheria vitakaposema kuwa msanii huyo kweli anahusika na shutuma hizo za uwizi.Kwa upande wa Lord Eyes amesema kuwa watu wanajua kuwa yeye ni mwanamuziki kwa muda wote na hajihusishi na maswala ya uwizi na ameomba mashabiki wavumilie kipindi hichi ambacho anapigania haki na ukweli utajulikana.

Wakili wa msanii Lord Eyes Peter Kibatala akieleza tukio zima la msanii Lord Eyes...MSIKILIZE akizungumzia tukio zima la msanii huyo na dhumuni la kuitisha mkutano na waandishi wa habari.


Msanii kutoka kundi la N2N Lord Eyes kwenye picha akizungumza na waandishi wa habari alianza kwa kumshukuru Mungu kwa kumpa nguvu katika kipindi hichi kigumu ambacho kesi ya kutuhumiwa kuhusika na wizi wa vifaa vya gari ikiendelea..MSIKILIZE...alichokisema.

 
NICK WAPILI AKIWA ANAFUNGUKA.
Habari kwa hisani ya Anna Peter.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.