Header Ads

Breaking News
recent

MATOKEO CCM: RAIS KIKWETE ACHAGULIWA TENA KUWA MWENYEKITI, MANGULA NA SHEIN MAKAMU MWENYEKITI.


Mwenyekiti wa CCM, Taifa, Jakaya Kikwete na Makamu wake wawili Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein (Zanzibar) na Philip Mangula (Bara) wakiwa meza kuu baada ya kutangazwa kushika nyandhifa zao.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM kwa kura  2395 kati ya 2397 zilizopigwa  ambazo ni sawa na asilimia 99.92% .

Matokeo ya nafasi za makamu mwenyekiti Zanzibar na Tanzania Bara yametangazwa rasmi, ambapo hakuna kura iliyoharibika hivyo wamepita kwa asilimia 100%.

Dr. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar amepita kwa idadi ya kura 2397 na hakukuwa na kura za hapana, hivyo kutangazwa rasmi kuwa ndio Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, wakati huo huo Philip Mangula amechaguliwa kwa kura 2397, hakuna zilizoharibika hivyo Mh. Mangula ndio Makamu Mwenyekiti mpya kwa upande wa Tanzania Bara.

Wajumbe wakiserebuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangazwa kuwa mshindi wa Uenyekiti wa CCM, Taifa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.