Header Ads

Breaking News
recent

MASTAA WA KIKE WATIA DOA KISOMO CHA STEVE NYERERE.

BAADHI ya mastaa wa kike Bongo wakiwemo Irene Uwoya, Sauda Mwilima, Salma Salmin ‘Sandra’ na Zuena Mohammed ‘Shilole’ wamekitia doa kisomo kilichoandaliwa na msanii mwenzao, Steven Mangere ‘Nyerere’ kufuatia kwenda kinyume na taratibu za dini ya Kiislam.

Steven Mengele ‘Steve Nyerere’ aliyeandaa kisomo hicho. 


Akizungumza na safu hii, ustadhi Juma Salum wa madrasa ya Kinondoni jijini Dar alisema, alichokifanya Steve Nyerere ni kitu kizuri ila kuna baadhi ya mastaa wa kike wameitia doa shughuli hiyo kwa kutofunika vichwa vyao.

“Kwenye Uislam mwanamke kuacha nywele zake wazi ni kosa, nimeshangaa kuona baadhi ya mastaa kwenye ile shughuli ya Steve wakiwa vichwa wazi na walikuwa ‘bize’ kuomba dua, kimsingi dua zao ni vigumu sana kupokelewa,” alisema ustadhi huyo.Hivi karibuni Steve Nyerere aliandaa kisomo na kuwaita maustadhi pamoja na wasanii wengine lengo likiwa ni kuwaombea mastaa waliotangulia mbele ya haki pamoja na kuondoa mikosi na balaa kwenye tasnia ya filamu Bongo. 

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.