Wednesday, July 23 2025

Header Ads

Watu wengi wahofiwa kufariki katika shambulio huko Ras Vegas, Marekani

Stori zilizo enea hadi sasa ni kwamba, Mzee wa miaka 64 aliwafyatulia risasi watu waliokuwa wakihudhuria tamasha la muziki na kuwaua watu takriban  zaidi ya 58

Watu wengine 515wanasemekana wanauguza majeraha. Hatahivyo kwa habari zilizopo ni kwamba mshambuliaji alijipiga risasi, polisi wanasema.

Watu takriban 22,000 walikuwa wanahudhuria tamasha ya muziki wa country usiku wa Jumapili katika eneo la wazi karibu na uwanja mdogo wa ndege wa Las Vegas.

Milio ya kwanza ya risasi ilisikika mwendo wa saa nne usiku saa za Las Vegas (05:00 GMT).

Mshambuliaji aliwafyatulia watu risasi kutoka ghorofa ya 32 katika hoteli ya Mandalay Bay na baadaye akajiua kwa kujipiga risasi.
BBC 
SUBSCRIBE YouTube account yetu upate video zaidi.

Leave a Comment

Powered by Blogger.