Baada ya stori kuenea toka 'Agost 23' Tylor Swift alipotangaza kuachia wimbo mpya na kusema pia album yake mpya kuwa inaitwa 'Reputation' basi kwa upande wa model Kim Kardashian, 36, usingizi ukakata.

Baada ya Kim kubaini huenda kinachokuja kuachiwa ni diss track kutoka kwa Taylor Swift, 27,basi mwana dada huyu alionekana kuweka chini stress na kuondoa attension ya mashabiki kwa Tylor na kutupia picha za nusu utupu wakati amekwenda kupata chakula cha mchana na dogo wake Khloe, 33, maeneo ya Studio City.
Kumbuka tifu na Tylor liliiva pale Kim alipofuma sauti ya siri ya mazungumzo ya Ty na mumewe Kanye West, 40, mwaka 2016, na Kim kuonekana kuisambaza mtandaoni.
Kwa sasa Tylor ameweka gumzo mtandaoni baada ya kuachia wimbo wake mpya unaoitwa ‘Look What You Made Me Do’ unaonekana kuwanyima usingizi.
Kim Kardashiani aonesha kukabiliana na ujio wa Tylor Swift kwa kuachia picha za nusu utupu
Reviewed by
KISHINDO TZ
on
Friday, August 25, 2017
Rating:
5
No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA