Header Ads

Breaking News
recent

TAMTHILIA YA HER MOTHERS DAUGHTER - PENZI LA MARGAUX NA ETHAN LAVUNJIKA.

Wiki nzima katika Tamthilia hii ya kusisimua, mambo yamekwenda katika hali ya msisimuko, ikiwa ni baada ya siri nyingi zilizokuwa zikifichwa kwa muda mrefu, kufichuka na hata baadhi ya wapenzi kupata misuko suko ya hapa na pale.

Mama yake Teresa sasa apata furaha ya moyo baada ya kumpata binti yake aliyekuwa akimtafuta kwa takribani miaka 17. Huku Julio naye baada ya kugundua kuwa Celyn ni binti yake anaamua kutafuta kila njia ili aweze kuwa na binti yake karibu, huku akijipanga jinsi ya kumuambia ukweli.

Katika harakati za Julio kutaka kujua ukweli kuhusu binti yake Celyn, familia yake yaanza kuingiwa na hofu kuwa huenda Julio anamahusiano na mwanamke mwingine. Hivyo mke wa Julio yani Beatrice anaanza kumfuatilia mmewe ikiwa ni baada ya mumewake kuanza kutumia muda mwingi nje akidangaya kuwa yuko ofisini.

Julio anaamua kumpangishia nyumba mpya mama yake Celyn, ingawa Celyn na Beatrice hawajajua swala hilo. Japokuwa Margaux ameanza kubaini kitu katika mwenendo wa baba yake katika familia yao Celyn.

Ukweli ni kwamba katika mahusiano ya kimapenzi Ethan anampenda sana Margaux, lakini kwasababu Celyn amekuwa msaada kwa mama yake Ethan, basi ameingia katika hisia za moyo wa Ethan pia. Liam ni kati ya wanaume wanaoonekana kuvumilia sasa katika hisia zao, ikiwa ni pale anapo onekana kumpenda Margaux, lakini haweki wazi.

Baada ya Margaux kuhisi kuchakachuliwa, sasa aamua kukaa mbali na Ethan na wenzake, lakini akiwa bado anafanya hivo, mara anamfuma Celyn akiwa na Liam akimueleza jinsi alivyotokea kumpenda mpenzi wa Margaux yani Ethan. Margaux anakasilika sana nakutaka kutomuona tena Celyn.

Celyn anaomba msamaha, lakini anakataliwa kata kata, Ethan anaamua kumfanyia surprise mpenzi wake Margaux ili kumaliza ugomvi wao. Anafanikiwa kumpata Margaux faragha na kumtaka apokee pete ya uchumba. Margaux anaonekana kufurahishwa na kitendo hicho, hivyo anakubali, ili baada ya hapo watoroke na kwenda kuishi mbali na wazazi.

Lakini mipango inatibuliwa na Liam na Celyn na kuwaonyesha wazazi wa Margaux sehemu walipoelekea. Wazazi wa Margaux naamua kumchukua binti yao kwa nguvu. Margaux anamlilia Ethan huku akisema nampenda Ethan, mniache niende na Ethan.

Baada ya Ethan kurudi nyumbani, kulizuka ugonvi mkubwa wa ngumi kati yake na Rio huku akimlaumu Liam kuwa ndiye aliyetibua mipango yote. Baada ya siku kadhaa, Ethan alimtembelea Margaux, na huko Margaux aliamua kumwambia  Ethan kuwa, mimi na wewe mahusiano baasi. Ethan hakuamini kwani ilimuma sana na kuamua kupita kwa kina Celyn kuwaambia.

Alipofika huko nako akamkuta Liam yuko na Celyn, akamueleza kuwa yeye na Margaux wameachana. Celyn kwa haraka akamkumbatia, kwani mbuzi amefia kwa muuza supu. Pembeni Liam alitabasamu kusikia habari hizo, kwani anajua kuwa huo ni mwanya mzuri wa kuumpata Margaux. Nini kitafuata? Endelea kufuatilia Tamthilia hii ya kusisimua.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.