Header Ads

Breaking News
recent

FILAMU YA WALANG HANGAN (MY ETERNAL) EPISODE YA 66 - SIRI NZITO ZAANZA KUFICHUKA- DANIEL NA KATERINA WARUDIANA.

Marco Montenegro na Emily Gidoti
Daniel amekwisha achiwa kutoka kizuizini kwani amekutwa hana hatia, lakini Katerina anafanya maamuzi magumu ya kukubari kuondoka na Nathan kwenda Dubai ili kunusuru maisha ya Daniel.

Daniel anaondoka hadi kwa mama yake Katarina na kumuulizia, lakini mama yake hakumficha ukweli, kwani alimpasulia kuwa, Nathan na Katerina wamekwenda air pot wakielekea  Marekani.

Daniel bila kupoteza muda aliwasha gari na kuelekea moja kwa moja air pot, lakini akiwa njiani alijaribu kumpigia Katerina, lakini Nathan aliinyakua simu na kuizima na kuitupa. Daniel hakukata taama kwani aliwasili air pot na kumkuta James akiwa tayari amekwisha muandalia passport, hivyo aliingia ndani moja kwa moja.

Ghafla Daniel alimuona Katerina na kumuita, wote waligeuka kwa taharuki nyusoni mwao, kwani hakuna hata mmoja ambaye alitegemea kumuona Daniel pale. Daniel alimsihi Katerina asiondoke na Nathan kwani kesi yake imekwisha.

Nathan anarukia mazungumzo yao na kumtaka Katarina waondoke huku akisema “Katerina ni mke wangu wa ndoa”, lakini ghafla Johanna alitinga ndani ya mjengo na kumsihi Katerina asiondoke na Nathan, kwani ndoa ya Nathan ni batili.

Kusikia usemi huo Katerina anapigwa na bumbu wazi kwani hakuwahi kusikia swala hilo, kuwa ndoa yake na Nathan ilikuwa ni batili, ikiwa ni baada ya kibali cha mchungaji cha kufungisha ndoa kucheleweshwa kukilipia upya.

Nathan anakasirika na kuanza kupasua vyombo ndani, Johanna anampigia simu baba yake na kumtaka aje haraka. Lakini Marco Montenegro na mama yake Margaret walipofika, siri ikavuja kwani Marco hakujua kuwa ndoa hiyo ilikuwa batili.

Miguel anatoroka jela na kurudi uraiani, sasa anapanga njama za kumuua Marco Montenegro ili amchukue Emily Gidot. Thomas nae anamkaba Nathan baada ya kujua kuwa ndoa yao ilikuwa ni batili.

Miguel anampigia simu Margaret na kumpa vitisho kwasababu ameshindwa kuwasambaratisha Emily na Marco. Margaret anampigia simu Ms Ihenya na kumueleza ukweli. Je Miguel mtu hatari sana atamuua Marco Montenegro? Je Daniel atadhurika tena? Nathan je ataamua nini juu ya Daniel na Katerina? Karibu kwa Dondoo nyingine hapa Asili Yetu Tanzania (The Best Swahili Blog) 

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.