Header Ads

Breaking News
recent

WAPENZI WA TAMTHILIA YA MARA CLARA WAINGIWA NA SMANZI KATIKA "EPISODE" YA 42.

Mchezo unaorushwa na kituo cha Staa Tv unaendelea kuchukua sura mpya baada ya kufanyika mazishi ya Mara, mmoja wa washiriki waliokuwa wakikonga nyoyo za mashabiki wengi.

MARA
Familia zote mbili zinazama katika dimbwi zito la kumpoteza binti yao, lakini siri nzito yazidi kutanda kati ya Gurly (baba wa sasa wa Clara) na washirika wake. Lakini pia polisi kama wameshtukia hivi mchezo unaoendelea, sasa wamtaka Clara kwa uchunguzi zaidi kuhusu kifo cha “Mara”, baba yake Clara hayuko tayari kuwakabidhi makachero wa polisi binti yake.

Kwa upande mwingine Clara anaanza kuchukua uwazi wa Mara kuwa karibu na mama yake wa zamani “Avira” na kumuahidi atakuwa nae karibu siku zote. Amenthe anarejea nyumbani usiku anamkuta Clara amelala na mama yake wa zamani “Avila”, hakubaliani na suala hilo anaamua kumrudisha kwao.

Japokuwa Clara na Gurly (Baba yake) waliweka agano na siri nzito ya kuzidi kummaliza Amanthe (Baba yake Mara) na kumtaifisha Avira, sasa mambo yaanza kuvuja wazi wazi baada ya makachero wa polisi kumfuata Clara wakitaka aongozane nao ili akafanyiwe mahojiano. Gurly anawazuia  lakini Clara anapaza sauti kuwa “hapana nitaongozana nao na nitawaeleza yote bila kuwaficha” baba yake anabaki ameduwaa, kwani Clara tayari amekwisha shtukia kuwa baba yake ndiye aliyehusika na mauaji ya “Mara”.

Nini kitaendelea? Tazama Star TV na pia tembelea ukurasa huu mara kwa mara kupata michapo ya tamthilia za mastaa hawa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.