TAMTHILIA YA “MARA CLARA” - "MARA" ANUSURIKA KIFO KATIKA "EPISODE" YA 43 LENITTA ASADIKIKA KUFARIKI.
Katika mwendelezo wa Tamthilia ya Mara Clara,
watazamaji wote walifahamu kuwa
muigizaji Mara kafariki katika Epsod 43 lakini ghafla Mara anaonekana, kumbe
aliye fariki hakuwa yeye.
![]() |
MARA |
Mara anajikuta yuko katika
familia ngeni ambayo haijui, lakini pia anajifanya amepoteza kumbu
kumbu, lakini kule kwao Clara anazidi kuongeza mazoea ya kutaka atumie muda
mwingi na mama yake wa zamani lakini bado ni vigumu.
Amanthe alimtuma mtu ili amfuatilie Gurlly lakini mbini hizo
zimetibuka baada ya Gurlly kushtukia mbinu hizo na kumbana mtu Yule na kuweka
siri wazi kuwa alitumwa na Amanthe kumfuatilia.
Gurlly anamfuata Amanthe nyumbani kwake na kumueleza kuhusu
mtu aliye muagiza amfuatilie, wote wanaghadhabika na kuzichapa mbele ya Avira.
Mama yake Gurlly ameanza kuwa na wasiwasi na mwanae kuwa
kuna siri nzito wamemficha kati yake na Clara na anadai kama itakuwa kweli basi
hajui maamuzi atakayo chukua. Huko nyumbani
kwa Amanthe kumewaka moto anadai lazima ampate muuwaji wa mwanae.
Japokuwa Clara na Gurly (Baba yake) waliweka agano na siri
nzito ya kuzidi kummaliza Amanthe (Baba yake Mara) na kumtaifisha Avira, sasa
mambo yaanza kuvuja wazi wazi baada ya makachero wa polisi kumfuata Clara
wakitaka aongozane nao ili akafanyiwe mahojiano.
Gurly anawazuia lakini Clara anapaza sauti kuwa “hapana nitaongozana nao na nitawaeleza yote bila kuwaficha” baba yake anabaki ameduwaa, kwani Clara tayari amekwisha shtukia kuwa baba yake ndiye aliyehusika na mauaji ya “Mara”.
Gurly anawazuia lakini Clara anapaza sauti kuwa “hapana nitaongozana nao na nitawaeleza yote bila kuwaficha” baba yake anabaki ameduwaa, kwani Clara tayari amekwisha shtukia kuwa baba yake ndiye aliyehusika na mauaji ya “Mara”.
Wameongozana yeye na baba yake pamoja na polisi hadi
kituoni, Clara amefunguka kuhusu walivyotekwa na mwanamke aliyekuwa akimpiga
mara kwa mara kule walikotekwa.
Clara azidi kujiwa na taswira zinazoashiria baba yake
kuhusika katika kifo cha Mara, anambana baba yake naye anakiri kumuuwa Mara.
Siri nzito inazidi kuvuja kwani Gurlly awapigia simu maaskari na kuwachongea
wenzake, wote wauwawa na kubakia mmoja ambaye amebanwa huku Gurlly akimuahidi
pesa ili asimtaje , sasa kibao chamgeukia
Christina kuwa ndiye aliyefanya mpango wote wa mauwaji.
Kule nyumbani mama yake Gurlly anaingia chumbani kwa Gurlly
na kupekua box na kupigwa na butwaa, kwani lilikuwa limejaa pesa.
Nini kitaendelea, tazama Star TV na karibu tena kwa
dondoo nyingine za tamthilia hii hapa
hapa.
No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA