Header Ads

Breaking News
recent

TAMTHILIA YA “MARA CLARA” EPISODE YA 46 – WAZAZI WA MARA WAGHUBIKWA NA WASI WASI, WAENDA KUUFANYIA MWILI VIPIMO VYA DNA.

"CLARA"

Clara anaachwa nyumbani na bibi yake, akimuhudumia lakini Clara anaonekana kukereka sana na bibi yake. Clara anamuacha na kwenda kwa mama yake wa zamani – Alvira.

Tayari Mara amerejea na kumkuta bibi yake akiwa ameachwa mwenyewe ndani, amuelezea jinsi alivyookolewa, lakini Mara na Christiani wanafanikiwa kuondoka kabla ya Garl kurudi.

Amante aenda anaamua kenda kwa Garl kwa siri ili kufanya uchunguzi wa kile kiatu kimoja polisi walichokikuta baada ya kurushiana risasi na Garl. Amante anafika kwa Garl na kumkuta Yule bibi mwenyewe na kumuambia kuwa Garl anahusika katika kifo cha mwanae.

Pia anafanikiwa kukiona kile kiatu, ghafla Garl anafika na kuanza kupigana na Amante. Huku kule Christian aendelea kumficha “Mara”.

Kwa upande wa Clara anang’ang’aniza kurudi kwao yani kwa Alvira. Clara hapendi kumuhudumia bibi yake na sasa amebeba mizigo yake na kurudi nyumbani na Alvira amempokea ikiwa ni mara ya pili baada ya Suzan kufuata huko.

Mara na Christian wanaenda kumuona bibi yao lakini wakiwa bado ndani Garl anaingia lakini wanafanikiwa kuondoka, nakumuacha Garl akimsaka Clara. 

Wanaamua kumfuata huko lakini Clara amewakana mbele ya Alvira na Amente na kumwambia Suzan kuwa “sikupendi kwasababu wewe si mama yangu” Garl aamua kupiga kimia na kumchukua Suzan hadi nyumbani.

Mama yake Christian amkuta MARA chumbani na kushikwa na uoga kama aliyeona mzuka uliofufuka. Anamuita Christian na kumueleza kuwa amemuona MARA, lakini Christian anapotezea kama vile ni ndoto. Kule kwao Clara kahamia kabisaa kana kwamba ndo kwao. Mama yake Christian ampigia simu Clara na kumueleza kuwa amemuona Mara kwake.

Mama yake Lenita anafika polisi na picha ya mwanae akimtafuta, kwa bahati Alvira na Clara walikuwa pale wanashikwa na butwaa, hisia zinaanza kuwajia kuwa huenda MARA alipona katika bomu. Wanaamua kwenda kuufanyia ule mwili walio uzika vipimo vya DNA.
Clara aamua kwenda kwa Kina Christian ili kufanya uchunguzi kama kweli “Mara” yungali hai? Huku Mara na Christian wakiwa tayari kuhamia katika eneo linguine. Je Clara atafanikiwa kukutana uso kwa uso na MARA?

Huku Garl aungana na wenzake na kuingia kwa kina Amante na kuripua bomu ili kupoteza muelekeo wa ushahidi.

Je nini kitaendelea. Tazama Star TV na karibu tena kwa dondoo  nyingine za tamthilia hii hapa hapa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.