Header Ads

Breaking News
recent

MASHABIKI WA TAMTHILIA YA “MARA CLARA” EPISODE YA 45 – MARA AREJEA NYUMBANI WAONANA NA GERLLY NINI KITATOKE?


Mama yake Gurlly amegundua mchezo wa Gurlly kumficha Christina pamoja na pesa nyingi alizoziona chini ya kitanda,bibi huyo ameamua kumfuatilia hadi alikomficha na kumuona Christina kwa macho yake.  
 Gurlly anasutwa na mama yake huku akimpangusa makofi mawili mashavuni, Gurlly kwa kushindwa kujizuia inabidi akubali kuwa ndiye aliyemuua “Mara” na anasema lazima ampate Avira kwasababu niwake tu, lazima wawe pamoja.

Kule kijijini Chistian azidi kumpa kampani ya kutosha Mara, japokuwa Mara anasisitiza warudi nyumbani kwao mjini. Kwa upande wa Amanthe wanahisa wa kampuni yake wanazidi kumbana kwasababu alitumia pesa nyingi bila ridhaa ya kampuni, na yote haya yanadhaminiwa na Christina ili kutupilia jela Amanth.
Mama yake Gurlly agoma kula na anadai ukweli aliouficha mwanae ndio utakao muuwa, bibi huyo anamkomalia Clara na kumlaumu huku akionekana kulia mda wote.

Amanthe anafuata na polisi na kupelekwa katika mahojiano kwa kufuja shilingi milioni 40, waandishi wanamsonga Amanthe na kumhoji. TV pia inatangaza kuwa aliyeandaa mbinu za kumuuwa Mara ni Christina.

Amanthe anampigia simu Christina na kumuomba wakutane ili waweze kuyazungumza, lakini Christina anamwambia kuwa muda ukifika wataonana lakini sasa haiwezekani.

Bibi huyo anamua kwenda kwa Amanthe na kuonekana kunajambo anataka kumuambia, lakini kabla hajafanya hivo, anaanguka chini na kupoteza fahamu, anakimbizwa hospitali, kumbe anaugonjwa wa kupooza.  Gerlly anapigiwa simu, wanakutana na Amanthe, Gerlly anamtwisha ngumi.

Gurll anakwenda nyumbani kuchukua pesa ili akalipe hospitali, lakini anakutana na box tupu alipokuwa ameziweka hazipo, anamkalipia Suzan akimuuliza ni nani amechukuwa pesa zake. Anataka kumpa kichapo, Clara  anamsaidia Suzan asipigwe.

Avira anaenda kumtembelea mama yake hospital, hawezi kuonge lakini anang’ang’ana kumueleza kitu lakini kabla Avira hajatambua kitu chochote, Gurlly anaingia na kutoa Avira inje.

Gurlly anadai ili amhamishe Christina kule aliko inabidi ampatie pesa. Christina anamuagiza aende kwake achukue pesa na vitu vya thamani ili aweze kumuhamisha. Lakini baada ya Garlly kuingia ndani tu gari la polisi likatia tim pale na kugundua kunamtu ndani. Wanaamua kuingia na kuanza kurushiana risasi, Gerlly anapata nafasi ya kutoroka huku akiwa amepigwa risasi.

Huko kijijini Mara anawasi wasi sana, anataka kurudi nyumbani lakini Christian anamzuia kwasababu huko hali bado si shwari. Christian na Mara waanza safari ya kurejea nyumbani. Wakati  Mara na Christian wanafika kumuona bibi yake wote wakiwa ndani, huko nje Gurlly anawasili. Je nini kitatokea? Au Gurlly ataamua kumteka Mara tena au?
Nini kitaendelea, tazama Star TV na karibu tena kwa dondoo  nyingine za tamthilia hii hapa hapa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.