Header Ads

Breaking News
recent

UKWELI KUHUSU VYAKULA KATIKA DINI YA KIKRISTO.


Nimekuwa nikisikia malumbano kadha wakadha mafundisho mbali mbali katika masuala ya vyakula, lakini hayo yote hutokana na mgawanyiko wa imani za watu mbali mbali wa dunia hii.

Lakini ni vyema wapendwa katika Kristo Bwana wetu wakarejea katika maandiko matakatifu na kuweza kuyatumia ipasavyo bila kujichanganya. Na nukuu vifungu hivi kutoka katika Biblia Takatifu;

"Basi Roho anena wazi wazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani,  kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.
Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani; kwakuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba (1Timotheo 4: 1-5)
VIGEZO VINGINE KATIKA VYAKULA TUPASAVYO KULA

Vitu vyote ni halali, bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo. Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake. Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza – uliza, kwaajili ya dhamiri; maana Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo.
Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza – uliza, kwaajili ya dhamiri. Lakini mtu akiwaambia, kitu hiki kimetolewa sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri. (1Wakorintho 10:23 – 28)
.
MWENDELEZO WA NUKUU ZA BIBLIA ZINAZOLENGA KUJENGA JAMII YETU, ZITAKUJIA ZAIDI HAPA HAPA.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.