Header Ads

Breaking News
recent

ZOEZI LA UTOAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA LAZINDULIWA RASMI LEO NA RAIS KIKWETE.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete leo amezindua rasmi zoezi la utoaji vitambulisho vya taifa katika sherehe zilizofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. 

Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali wakiwemo marais wastaafu Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Amani Abeid Karume. Baada ya zoezi la uzinduzi, Rais Kikwete aliwakabidhi baadhi ya viongozi vitambulisho vyao vya taifa.


Rais Kikwete akimkabidhi kitambulisho rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi.


Akimkabidhi kitambulisho rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.


Wasanii mbalimbali wakiongozwa na Muumin Mwijuma (wa pili kushoto) na Isha Mashauzi (wa pili kulia) kutoa burudani wakati wa sherehe hizo.


Wasanii kutoka THT wakiongozwa na Linah Sanga (kulia) wakizikonga nyoyo za wageni waliohudhuria zoezi hilo.

(PICHA NA MAKONGORO OGING' / GPL)

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.