ASKOFU THOMAS LAIZIER WA KANISA LA KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI AMEFARIKI DUNIA.
Askofu wa kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania dayosisi ya kaskazini kati Askofu Thomas
lazier amefariki Dunia jioni ya leo.
Habari ambazo zimethibitishwa na katibu Mkuu wa dayosisi
hiyo Israel Ole Karyongi zimesema kuwa askofu alikumbwa na mauiti majira ya
saa 12 za jioni ya leo.
“Ni kweli baba Askofu amepita na tuko katika hali ya dharura
ngumu na tungependa mtuachie nafasi ili tuwape taarifa juu ya msiba huu
kesho”alisema Karyongi akizungumza kwa njia ya simu .
Askofu lazier ndiye
askofu wa kwanza wa na mwanzilishi wa dayosisi hiyo ambayo awali ilikuwa ikiitwa dayossi
Mkoani Arusha kabla ya mwaka juzi kubalishw ajina na kuitwa dayosisi ya
kaskazini kati.
Ni msiba mkubwa mno katika Mkoa wa Arusha kutokana na askofu
huyo kupata umaarufu katika kazi zake za
kiroho na kijamii husasan jamii ya kabila la wamasai.
Anatajwa kushiriki katika kuendeleza jamii hiyo kielimu kwa
kubuni na kuanzisha shule zaidi ya ishirini za sekondari zikiwemo maalum kwa
ajili ya watoto wa kike.
Habari zaidi na CHARLES NGEREZA

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema,Amen
ReplyDelete