PRECISION AIR YAZINDUA SAFARI ZA KIGOMA
· Sasa wateja wake kulipa Sh 199,000 kwa kila safari kutoka
Dar hadi Kigoma kila siku
· Safari zote kufanyika mapema kabla ya safari za treni
kutoka stesheni ya Dar es Salaam
. Sasa idadi ya safari za shirika letu zafikia 19
DAR ES SALAAM, JANUARI 31, 2013 – SHIRIKA la ndege la
Precision Air (PW) limezindua safari zake za kila siku kutoka Dar es Salaam
kwenda Kigoma kupitia Kigoma Airport kwa kutumia ndege yake aina ya ATR 42 na
hivyo kufanya idadi ya safari za shirika hilo kwenye soko kufikia 19.
Uzinduzi wa safari za Kigoma utawezesha shirika hilo kufanya
safari zake kila siku kwenda Kigoma kwa kutumia ndege yake aina ya ATR 42-600.
Maendeleo haya yanakuja miezi michache baada ya uzinduzi wa safari mpya mkoani
Mbeya.
Ndege hiyo itakayofanya safari za kila siku kwa kutumia
dakika 60 kwa kupitia Mwanza. Wakati safari za kutoka Dar es Salaam kwenda
Kigoma kupitia Mwanza zitafanyika siku za Jumatatu, Jumatano Ijumaa, Jumamosi
na Jumapili kuanzia saa 12 asubuhi na kufika Mwanza saa 7.30 asubuhi na
kuunganisha Kigoma saa 4 asubuhi ya siku hiyo na kufika Kigoma saa 11.10 asubuhi.
Kuondoka Kigoma kwa siku hiyo itakuwa ni kuanzia saa 11.40
asubuhi na kufika Mwanza saa 12.50 mchana na kuunganisha Dar es Salaam saa
13.00 mchana na kufika mwisho w safari yake saa 15.00 alasili.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Masoko wa Precision Air, Linda Chiza,
alisema kuwa safari hizo mpya zitatoa fursa kwa wafanyabiashara wengi na
watalii kuweza kutalii kwenye vivutio mbalimbali vya kitalii mkoani Kigoma.
“Tunayofuraha kuzindua safari hizi za Kigoma na tunaamini
kwamba nyongeza hii ya safari ni dhahiri itaweza kuchangia ongezeko la uchumi
katika mkoa wa Kigoma,” anaeleza Chiza
Alieleza pia kuwa nauli ya kutoka Dar es Salaam-Kigoma ni
kiasi cha Shilingi 349, 000 ikiwa ni safari ya kwenda na kurudi. Huku gharama
ya nauli Dar es Salaam kwenda Kigoma pekee ni Shilingi 199,000.
Mkoa wa Kigoma una wastani wa watu takribani milioni 2
ambapo mkoa huo una pakana na nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
(DRC).
Kutokana na hilo, safari hizo za Kigoma zitakuza biashara na
kuwanufaisha wafanyabiashara ndani ya nchi na nchi jirani ya DRC. Safari hizo
za Kigoma zinatarajiwa kukuza sekta ya utalii nchini.
Kigoma yenye bandari ya Lake Tanganyika ni moja ya bandari
zilizogubikwa na shughuli nyingi ambapo kihistoria ilikuwa ndio bandari pekee
yenye reli inayounganisha (mji wa Kalemie nchini Kongo), na vilevile kupitia
reli hiyo bandari ya mkoa huo inaunganishwa moja kwa moja na bandari ya
Dar-es-Salaam kwa ustawi wa mikoa hiyo na watu wake.

No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA