MASTAA WA BONGO NDANI YA MATUKIO YA KUSIKITISHA KWA MWAKA MZIMA WA 2012.
![]() |
| Steven Kanumba na Mzee Kipara enzi za uhai wao. |
Mwaka 2012 umepewa jina la mwaka wa shetani katika sanaa ya Kibongo baada ya kufariki kwa vichwa kibao katika tasnia mbalimbali.
MZEE KIPARA
Mwanzoni mwa mwezi Januari, mwigizaji wa siku nyingi Bongo, Said Fundi ‘Mzee Kipara’ alifariki dunia akiwa kwenye nyumba ya Kundi la Sanaa la Kaole, Kigogo jijini Dar baada ya kusumbuliwa na maradhi mbalimbali yaliyomuandama kwa muda mrefu na utu uzima.
KANUMBA
Aprili 7, 2012, hali haikuwa shwari katika tasnia ya filamu za Kibongo baada ya kufariki kwa ‘legendary’, Steven Kanumba aliyepoteza uhai ghafla baada ya kudondoka nyumbani kwake maeneo ya Hoteli ya Vatican, Sinza jijini Dar.
Mchezaji wa Simba, Patrick Mafisango alivyo pata ajali na
gari yake Toyota Crestar Gx 100 hadi umauti wake ulipo mfika kwenye ajali hiyo
Mwezi Mei, mwaka huu, sekta ya michezo nayo ilikumbwa na simanzi baada ya mchezaji wa Simba, Patrick Mafisango kufariki dunia kwa ajali iliyotokea maeneo ya Tazara, Dar, wakati akijaribu kumkwepa mwendesha bodaboda ambapo gari lake liliingia mtaroni na hapo ndipo alipopoteza maisha.
![]() |
Mwezi Novemba kilio kilisikika kwenye muziki wa Taarab baada ya kufariki ghafla kwa staa wa Kundi la Tanzania One Theater (TOT), Mariam Khamis ‘Paka Mapepe’ alipokuwa akijifungua.

MLOPELO
Pia Novemba mwaka huu, mwigizaji aliyepata umaarufu mkubwa enzi za Kaole Sanaa Group kupitia runinga ya ITV, Khalid Mohamed ‘Mlopelo’ alifariki dunia kwenye Hospitali ya Temeke, Dar baada ya kuwa na maumivu ya mwili kwa muda mrefu.
JOHN MAGANGA
Kuonesha kuwa mwezi Novemba bundi alikuwa ameng’ang’ania tasnia ya filamu za Kibongo, pia alifariki mwigizaji John Stephano Maganga baada ya kuugua kwa muda mfupi na kulazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar.
SHARO MILIONEA
Mwenzi huohuo wa gundu, mwigizaji na mwanamuziki, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’, alifariki dunia kutokana na ajali ya gari iliyotokea usiku katika eneo la Maguzoni Songa katikati ya Segera na Muheza mkoani Tanga alipokuwa safarini kuelekea nyumbani kwao Muheza kumpelekea mama yake fedha za matumizi.
LULU OSCAR
Pia ndani ya mwezi huohuo, aliyekuwa Mtangazaji wa Kipindi cha Pepeta Afrika kunako SibukaTV, Dar, Lulu Oscar alifariki ghafla akiwa nyumbani kwao Mbezi-Kwayusuf, Dar baada ya kuzidiwa kwa kubanwa na kifua.
AMINA SINGO
Mwezi Desemba, fani ya utangazaji nayo ilipata pigo baada ya kuondokewa na aliyekuwa Mtangazaji wa Kipindi cha Afro-Vibes cha Times FM, Dar, Amina Singo aliyekuwa akiugua kwa muda mrefu.
Stori: Sifael Paul (Globa Publishers).



No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA