Header Ads

Breaking News
recent

WAKRISTO NAO WATAKA MACHINJIO YAO, WADAI HUPATA SHIDA.


BAADHI ya wananchi wa Wilaya ya Busega wametaka kuwepo na machinjio ya Wakristo peke yao kwani hivi sasa wanapa shida wanapochinja mifugo yao ambayo wakati mwingine hukamatwa.

Wakitoa maoni kwenye kata mbalimbali juu ya uandikwaji  wa Katiba mpya, walisema kutoka na kutokuwepo kwa machinjio ya Wakristo, baadhi ya maduka ya nyama yamekuwa yakichomwa kutokana na kudhaniwa yanauza nyama ambazo mifugo yake ilichichwa na Wakristo.

“Katiba ikubali kuwa waumini wachinje wanyama wao, tofauti na kuwa kwamba machinjio yote yameshikwa na watu wa dini moja tu,” alisema Iswambula Kiswaga  mkazi wa kata ya Kalemela

Pia alisema kuwa, katiba hiyo ianishe siku ya kufanyika kwa chaguzi mbalimbali ambapo siku hizo zisiwe zile za kuabudu.

“Uchaguzi uwe unafanyika kati ya siku ya Jumatatu, Jumanne, Jumatano au Alhamisi jambo analosema litaongeza idadi ya watu wanaopiga kura, tofauti na sasa ambapo maelfu wanajitokeza kujiandikisha lakini siku ya kupiga kura ya wanajitokeza wachache.

Naye Enock Kindika, alisema kuwa Rais apunguziwe muda wa kutawala, awe na vipindi viwili vya miaka  miwili  na siyo vipindi viwili vya miaka mitano.

Anasema kuwa, kwa muda uliopo sasa unawafanya wananchi wateseke kama walifanya makosa katika kumchagua kiongozi huyo wa nchi.

Kwa upande wa Musa Simba (18), mkazi wa  Kalemela, alisema kuwa idadi ya wabunge ipunguzwe, na pia kuwafuta wabunge wa kuteuliwa na Viti Maalumu kwa kile alichosema kazi yao haionekani.

“Hata vyama vipunguzwe, tuwe na vyama viwili tu vitakavyoshindana kwenye uchaguzi,” alisema.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.