Header Ads

Breaking News
recent

'NAY WA MITEGO' AMKANA 'NISHA', ADAI HAYUPO KWENYE MAHUSIANO NA MWANAMKE YEYOTE.


WAKATI watanzania wengi wakiamini kuwa msanii Ney Wa Mitego, yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na mwanadada wa kwenye tasnia ya filamu Salma Jabu ’Nisha’, mkali huyo wa ngoma ya ‘Wamenichokoza’, amekanusha uwepo wake kwenye mahusiano na mwanamke yeyote na kudai kuwa kwa sasa ana marafiki tu wa kike wa kubadilishana mawazo na si wapenzi au mpenzi kama watu wanavyodai.

Hata hivyo kauli ya msanii huyo inaweza kuzua utata mkubwa kwani mashabiki wake wengi wanajua kuwa mpenzi wake ni mwanadada huyo wa bongo movie ingawa tangu kutoka kwa habari hizo hakuwahi kuzungumza lolote juu ya mahusiano hayo kama ni kweli.

“Hapana kwa sasa sina mpenzi, nimeshatoka na wanawake kadhaa hilo lipo wazi lakini kwa sasa natafuta yule mpenzi mwenye tabia njema,” alisema.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.