Header Ads

Breaking News
recent

MAKEKE AFRIKA KOLEKSHENI INAKULETEA MITINDO NA UBUNIFU MPYA TANZANIA.

Asili Yetu Tanzania.Copyright

 KIOTA KIPYA CHA MASWALA YA UBUNIFU NA MTINDO
Mdau leo naomba kukutambulisha kwako kijana wa Kitanzania anaekuja kwa kasi katika fani ya Ubunifu na Mitindo, Kwa majina anaitwa JOCKTAN MALULI akiwa chini ya Kiota Chake cha MAKEKE AFRIKA KOLEKSHENI ambapo ameamua kuleta mapinduzi makubwa katika kilinge cha Mitindo na Ubunifu hapa Tanzania lakini pia nje ya Mipaka ya Tanzania.

Inawezekana kabisa jina la kijana na kazi za kijana huyu mwenye MAKEKE mengi zikawa hazijulikani sana, JOCKTAN MALULI maarufu kwa jina la MAKEKE ni mhitimu wa shahada ya Sanaa ya Uchoraji na Ubunifu katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Akiamini kabisa kwamba soko la sanaa ya Ubunifu na Mitndo likiwa na Ushindani mkubwa hapa nchi MAKEKE anajivunia uwezo wake mkubwa katika fani hii akitumia mbinu mbalimbali zilizo kichwani mwake kwani si tu kipaji pekee alichonacho bali MAKEKE ana elimu ya sanaa hii ya Mitindo.

Mpaka sasa MAKEKE AFRIKA KOLEKSHENI imeshashiriki katika Matamasha mbalimbali ya Ubunifu na Urembo ikiwa pamoja na Redds Fashion Mbeya, Redds Fashion Dodoma, Dom Fashion Night, na UDOM Fashion Soul.

Kijana huyu ameshafanya kazi pamoja na Magwiji wa sanaa hii ya Ubunifu na Mitindo hapa nchini kama AILINDA SAWE, kwa sasa MAKEKE anafanya kazi na gwiji mwengine Mustafa Hassanali akiwa ni Graphics Designer. Kwa taarifa zake nyingi Faceboo: MAKEKE AFRIKA KOLEKSHENI; Simu : +255754411889

BAADHI YA KAZI ZA MAKEKE AFRIKA KOLEKSHENI

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.