AUNT EZELIEL AOLEWA BAADA YA MISUKO SUKO MINGI KUPITA.
Asili Yetu Tanzania.Copyright
![]() |
| Aunt Ezekiel pichani akionekana na tabasamu wakati wa harusi yake. |
HATIMAYE msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel amefunga ndoa
Oktoba 18, mwaka huu ambapo shughuli hiyo iliyofanyika Mwananyamala jijini Dar
ilihudhuriwa na ndugu, jamaa na rafiki zake.
Aunt alifunga ndoa ya Kiislam na mchumba wake wa siku nyingi
aitwaye Sunday Demonte anayefanya shughuli zake za kibiashara huko Dubai.
Aunt kabla ya tukio hilo alisema ni
kweli amelazimika kutimiza zoezi hilo
ili maisha mengine baada ya ndoa yaweze kuendelea.
“Ni kweli nimefunga ndoa leo ila Sunday hayupo,
atawakilishwa na ndugu yake na sherehe kubwa itafanyika huko Dubai,”alisema Aunt.
Na Imelda Mtema (Global Publishers)

No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA