Header Ads

Breaking News
recent

ASILI YETU BLOG: MWALIMU MKUU WA SHULE YA SEKONDARI YA ILBORU ARUSHA, ASIMAMISHWA KAZI.

Asili Yetu © All rights reserved


SERIKALI imemsimamisha kazi, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ilboru, Jovinus Mutabuzi, kufuatia madai ya tuhuma mbalimbali za fedhana matumizi mabaya ya madaraka yaliyosababisha wanafunzi  kuandamana hadi ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakishinikiza ang’olewe kutokana na tuhuma za ulaji fedha na matumizi mabaya ya madaraka.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, anayeshughulikia Elimu, Kasimu Majaliwa, alitangaza uamuzi huojana  baada ya kusikiliza madai ya wanafunzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika shuleni hapo.
Pamoja na kusimamishwa kazi, Naibu Waziri Majaliwa, amemteua Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo ya wanafunzi wenye vipaji maalum, iliyopo wilayani Arumeru, mkoani Arusha, Lorna Nteles, kukaimu nafasi ya Mwalimu Mkuu.

Katika hatua nyingine, Majaliwa, amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Arusha, Halfa Hida, kuteua mkaguzi wa ndani kufanya uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili Mutabuzi, ikiwemo ya kutumia stakabadhi bandia anazodaiwa kuhalalisha malipo ya wanafunzi.

Katika mkutano wake wa hadhara na wanafunzi hao, Majaliwa, alibaini kuwa hoja zao ikiwemo ya matumizi mabaya ya fedha kiasi cha Sh.milioni 800 kuziingiza kwenye Chama cha Kuweka na Kukopa (SACCOS) ambapo alikuwa akizikopesha kwa riba kwa walimu na watumishi wa shule hiyo.
Jumatatu wiki hii, wanafunzi wa shule hiyo waliandamana hadi ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, kwa lengo la kushinikiza kung’olewa kwa mkuu huyo, ambapo pamoja na mambo mengine walidai kuwa ameshiriki kuifanya shule hiyo kudorora kitaaluma na kuwadhalilisha wanafunzi kwa kuwaita mashoga. 

Mkuu wa Mkoa Magesa aliwasihi wanafunzi hao kurejea shuleni na kuendelea na masomo wakati suala lao likishughulikiwa, hata hivyo, baaada ya kurudi shuleni walianzaisha mgomo wa kutoingia darasani ikiwemo kutokula chakula cha shule hiyo.
Hatua  hiyo,  ilimlazimu Naibu Waziri, kufika shuleni hapo na kuwasikiliza wanafunzi hao, ambapo kabla ya kufanya mkutano alitembelea maeneo yote yanayolalamikiwa na wanafunzi hao ikiwemo, jiko la chakula, mabweni pamoja na choo cha matundu mawili kinachodai
kujengwa kwa Sh. milioni 25.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara shuleni hapo, Majaliwa aliwasihi wanafunzi hao kutovunja sheria kwa kuitisha migomo na maandamano yasiyo rasmi huku akimtaka makamu wa shule hiyo kusimamia nidhamu kwa wanafunzi hao.

Naibu waziri akiwa ameandamana na askari wa kikosi cha  kutuliza ghasia waliokuwa na mabomu na silaha za moto, alilazimika kutumia saa zaidi ya tano kutoa ufafanuzi wa madai ya wanafunzi hao ambao muda wote walionyesha kumsikiliza kwa makini huku hoja yao kubwa wakidai hawamtaki mkuu huyo.

Hata hivyo,  Mjaliwa alikerwa na mabango aliyoyakuta yamebandikwa kwenye kuta katika majengo yote ya shule yakiwa na ujumbe mbalimbaliwa kumpinga Mwalimu Mutabuzi huku baadhi yake yakiwa yamechorwa vikaragosi vinavyomfananisha utawala wa  mkuu huyo na ule wa marehemu Nduli Idd Amini dada wa Uganda.

Pamoja na kuwasihi kuwa wawe wavumilivu wakati hatua zaidi zikichukuliwa lakini walipaza sauti wakidai kuwa hawapo tayari kuingia darasani bila kuondolewa kwa mkuu wao hali iliyomlazimu Naibu Waziri kutamka kuwa amemsimamisha kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo, hali iliyoamsha shangwe na nderemo kwa wanafunzi hao.

Naibu waziri amepiga marufuku michango isiyo na tija mashuleni, matumizi ya simu za mkononi kwa wanafunzi, adhabu za malipo ya fedha, matumizi ya M-Pesa mashuleni pamoja na kuziagiza bodi za shule kutatua matatizo ya wanafunzi pale yanapoibuka kabla ya kuleta madhara

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.