Header Ads

Breaking News
recent

MSANII NISHER BYEBEE AKIWA NDANI YA TRIPLE A RADIO ARUSHA.

Baada ya msanii mkali mithiri ya Usher Raymond " NISHER BYEBEE" kudondoka ndani ya mjengo wa 88.5 Triple A Fm, tulipiga story na kufahamu mengi kuhusiana na muziki anaoufanya.
Nisher & Dj Mark ndani ya "The beat 120"
Victor Machota & Nisher ndani ya mjengo
Kutoka kushoto ni Station Manager "Borry Bthepilot" akiwa na artist Nisher Byebee ndani ya 88.5
Dj Askof kama kawaida yake aligonga mawe ya kijanja, mwenyewe si unaona???
"KENY"kutoka kushoto huyu ndiye main hoster wa kipindi cha "The Beat 120" ndani ya live interview na msanii "Nisher"

 Wakati tunapiga story za hapa na pale mtu mzima "Nisher Byebee" alifunguka kama ifuatavyo.....
Unaweza ukanipa inshort about your music? coz nataka kupublish now kwenye blog?

"Ok what would u like to know kuhusu my music?" 

Umeanza lini music,unaulbam au single ngapi? Zinaitwaje, ume release ipi na unamatarajio gani kwa baadae?

"Music nimeanza toka nikiwa na umri wa miaka 7, lakini nikaanza kua serious zaidi mwaka 1998 hadi leo hii, hii ni baada yakumfahamu na kuvutiwa na mwanamuziki wa kimarekani Usher Raymond IV ... Album iko jikoni... Nyimbo zangu natunga nakuandika mwenyewe pamoja na kuziproduce kwenye Studio yangu "Nisher Records" chini ya "Nisher Entertainment", Nilitoka na single iitwayo "Nisher" lakini saivi nimekuja na track inaitwa "Boyfriend"
Nategemea kujakuwa Icon Wa Tanzania kama mwana muziki, Mwana Mitindo na Mwingizaji filamu.... Nataka kuacha alama yangu katika nchi hii na nje! Napenda kujulikana badae kama mtu aliye badili ama kugeuza soko la Mziki wa Tanzania!"

Ok! Style yako kido iko kama unique hapa bongo, je unahisi unakompetition na wasanii gani wa hapapa bongo?

"Watanzani wajipange mana ndo nimeingia Rasmi! Video yangu itatoka Muda wowote kuanzia sasa hivi... Macho yote yawe facebook na kwenye Blog yangu... www.nisherthestar.blogspot.com"


Katika video yako tutegemee sura zipi,na itafanyikia katika mazingira yapi?...producer?

"Nadhani kwa habari ya competition siwezi kujua sana manake spendi kujifanya mjuaji, wanamuziki na ma Mc wanazaliwa kwa sekunde bongo, sio kwa dakika...Hivyo nawaachia mashabiki waamue nani mkali!"

Poa! Labda unachochote cha kuongeza kwa mashabiki wako?......... You have a girfrend or wyfe! hahaaa!!

"Kwanza video yangu ya kwanza ntaidirect mwenyewe, nataka kufanya kitu kipya kwa habari ya Mwonekano, nataka kutoa kitu ambacho hakija zieleka Tanzania! Ningependa Marafiki zangu Mastar mbali mbali wawepo kwenye video hiyo!"

Mastaar kama??

"Bado Sjaamua, Lakini ningependa kama angekuwepo, AY, Mwana FA, Lamar (Fish Crab), Ngwea, Chidi Benz nawengine Kibao! Pia mastar wa Movie.... Nataka Video yangu isiwe tu kuhusu muziki iwe ni Hadithi ya Kusimuliwa na kutazamwa hata miaka 10 baadae ..
Staki kufanya kitu cha mpito kama waliopo saivi! Nataka kuweka historia ya kidumu miaka mingi! Nilijifunza kwa Baba yangu.... Kwangu mziki sio kazi ni Hobby tu, lakini tofauti nikwamba sitanii, nafanya kweli!"
 
Bilashaka umewahi kuwa nje ya +255, je unaona nini ambacho kinakwamisha game letu la mziki kuendelea kudidimia tofauti na nchi nyingine?

"Yap nimesha safiri nchi nyingi, nimekua America, South Africa, Egypt, UAE (Dubai) na Europe.... Tatizo letu kubwa au dogo nikwamba hatu taki ku-Push the limits za kimuziki... Tanzania imeridhika na kinachoitwa 'bongo fleva' na kusahau kwamba ushindani niwa-dunia nzima sio hapa nyumbani tu! Ndomana watu kama mimi na wenzangu kama Lamar (fish crab) tunataka kubadilisha Game ilikuongeza ushindani na ufanisi zaidi!
Utanitumia jina la blog yako iliniirushe kwenye post zangu washkaji waicheck au vip?"

Pamoja mzazi!

"Pa1 bro!!"

Pouuwa!
Namengine zaidi yatakujia hivi karibuni so stay tune!!!!!!!!

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.