Header Ads

Breaking News
recent

Watafiti wabaini kuwa Mbwa Mwitu hufanya maamuzi kwa kutumia chafya

Mbwa mwitu hufanya maamuzi yao kwa kupiga kura kupitia kupiga chafya kwa mujibu wa utafiti mpya.

Utafiti huo wa pamoja uliofanywa na wasomi kutoka Swansea, Australia na Marekani ulifuatilia mbwa mwitu walio kwenye hatari ya kuangamia nchini Botswana

Waligundua kuwa mbwa walitumia chafya kuamua wakati wanaelekea kuwinda baada ya kufanya mikutano inayofahamika kuwa mikutano ya kijamii.
Awali ilikuwa ikifikiriwa kuwa mbwa hao ambao ni familia ya wanyama walio kwenye hatari zaidi ya kuangamia duniani, walikuwa wakipiga chafya ya kawaida.

Lakini wakati watafiti wakirekodi mikutano 68 ya mbwa mwitu waligundua kuwa, wakati walipiga chafya zaidi walikuwa wakiondoka na kuanza  kuwinda.

Dr King anasema kuwa chafya hiyo ni lazima ifike kiwango fulani kabla ya wao kuamua kufanya kitu.

Pia utafiti huo uligundua baadhi ya chafya huwa na uzito kuliko zingine.
Stori na BBC 

Endelea kufuatilia dondoo kibao za KITOFAUTI duniani kupitia blog yetu ya ASILI YETU TANZANIA. Pia subscribe You Tube account yetu  kupata update kibao.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.