Header Ads

Breaking News
recent

VITUKO: Mke aruhusiwa kumuacha mumewe, kisa nyumba yao haina choo cha ndani.

Mahakama kaskazini mwa India, imempa ruhusa mwanamke katika jimbo la Rajasthan ruhusa aachwe na mumewe, kwa sababu nyumba yao haina choo.

Wakili wa mke, alidai kuwa kwa vile mume hakumjengea choo ndani ya nyumba, katika miaka mitano ya ndoa, basi huo ni ukatili.

Jaji alisema kwenda kufanya haja nje ni kitu cha aibu, na ni kumuadhibu mwanamke, kukosa kumuweka mwanamke pahala salama anapokwenda haja.

Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF linasema kuwa karibu nusu ya watu nchini India, karibu watu milioni 600 hawana choo.

Mwaka uliopita mwanamke alikataa kuolewa na mwanamume mmoja katika jimbo la Uttar Pradesh baada ya mwanamume kukataa kujenga choo.
Na bbc

Endelea kufuatilia dondoo kibao za KITOFAUTI duniani kupitia blog yetu ya ASILI YETU TANZANIA. Pia subscribe You Tube account yetu  kupata update kibao.  

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.