Header Ads

Breaking News
recent

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA YA KUINGIA KATIKA NDOA.



Asanteni tena kwa kujumuika nasi hapa katika ukurasa huu unaolenga kuwafungua watu katika maswala mbali mbali ya kijamii, yanayokwamisha maendeleo ya watu pamoja na kusambalatisha mahusiano ya watu.

Leo tunaangalia mambo ya kuzingatia kabla ya kuingia katika ndoa, na hapa wengi huenda nikaenda tofauti nao, lakini ni jukumu langu kuelimisha jamii na sio kuifurahisha tuu. Kila mtu anafahamu neno mahusiano ya kirafiki kati ya jinsia mbili tofauti.

Kabla ya kuingia katika ndoa, lazima ufanye urafiki na mtu unayetaka kumuoa au kuolewa naye, ili uweze kubaini tabia na mwenendo wake kama unaendana na wakwako, au anamatatizo gani ya kiafya au kiukoo pia.

Tumekuwa tukikimbilia kufanya mapenzi ili kupima uwezo wa injini kama inahimili safari na kusahau usukani wa gari, kwani gari haliwezi kukufikisha pale unapotaka kwenda bila ya kuwa na uskani (staring).

Kwa wachumba na wasio wachumba yani Girlfriend na Boyfriend, kama kweli unampango wa kumuoa au kuolewa, ni vyema usiendekeze kufanya mapenzi na mwenzi wako, kwani kufanya mapenzi na rafiki yako unayetarajia kumuoa au kuolewa naye, hupunguza upendo au hisia na shauku ya kutaka kuishi kama mume na mke kwa baadae.

Kama kimwili utampa mpenzi wako kila kitu anachokitaka, then nini kitakuwa kimebakia katika mwili wako ambacho atakuwa na shauku ya kutaka kukipata? Hisia kubwa ya ndoa ni mapenzi na kupata watoto, na ndio maana wasichana wengi wanachelewa kuolewa au hata hawawezi kuolewa kwasababu hawana mipaka katika maamuzi ya mapenzi.

Kuna njia nyingi za kumridhisha mpenzi wako na akasahau kukuomba kufanya.....Endelea  hapa Bofya JITAMBUE KWANZA

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.