Header Ads

Breaking News
recent

TAMTHILIA YA “WALANG WANGGAN” EPISODE YA 1&2 – MAHUSIANO YA “MARCO” NA “EMILY” YAWEKEWA VIKWAZO.


Baada ya Mara na Clara kufanya  vizuri, sasa ni Emily na Marco ambao wanatokea kupendana na kulishana viapo vya kuto umizana katika mahusiano yao. Lakini mama yake MARCO tayari ameanza kuweka vikwazo kibao.

MARCO ni kijana pekee anayetoka katika familia ya kitajiri ya mzee Joseph huku  mama yake anaitwa “Margret”. Marco anatokea kumpenda mmoja wa  watumishi wa mama yake anayefahamika kama EMILY.

EMILY ni binti anayetoka katika familia masikini, huku akiwa akiishi na baba yake. Emily ni mfanyakazi wa familia ya MARCO.  Siku moja familia ya Marco waliaandaa sherehe nyumbani kwao na kuwaalika watu wengi katika sherehe hiyo huku Emily akiwa mmoja wa wahudumu.

Emily akiwa amebeba vyakula akipeleka katika sherehe, mara alimuona Marco akikatiza kwa mbali, alikuwa kama amepigwa na butwaa kidogo huku akiendelea kujongea. Wakati akiliopogeuka tu wakagongana na mama yake Marco ambaye ni boss wake, alikasilika sana kwani alionekana kuaibika mbele.

Siku Marco anaenda kumtambulisha Emily kwa mama yake, ilikuwa tofauti kwani mama yake alimkatalia Marco kutaka kumuoa Emmily, kwani aliamini kuwa Emily amempenda Marco kwasababu ya pesa alizonazo.

Tayari Margret mama yake Marco anatinga nyumbani kwao Emily na kumuachia vitisho kibao ikiwemo kunyang’anywa ardhi yao.

Baada ya mama yake Marco, kuiandama familia yao Emily, sasa baba yake Emily anaamua kuondoka na binti  yake katika mji jirani ili kuepukana na zahama ya Margret. Lakini mama yake Marco anamtuma mtu awafuatilie na kuwabambikizia uzushi ili baba yake Emily awekwe jela.

Mtu aliyetumwa anafanikiwa kufanya hivyo, isipokuwa inakuwa kinyume, kwani baba yake  Emily wakiwa mahakamani anaanguka na kuzimia, matokeo yake Emily ndiye anapelekwa jela ambapo alionekana ni mja mzito baada ya siku chache kufika jela.

Mipango yote hiyo ya Margret, Marco hakujua napia hakujua kama Emily alikuwa na mimba yake, sipokuwa alipata taarifa ya Emily kuwa jela ambapo aliweza kumtembelea, lakini Emily alimtimua.

Marco na Jenny wanafunga ndoa baada ya Emily kumsusia Marco, huku Emily anajifungua mtoto wa kiume ambae inasemekana amefariki mara baada ya kuzaliwa. Je, kunaukweli wowote kuhusiana na motto kufariki au ni kiini macho tu?

                      Je nini kitaendelea?  Karibu tena kwa dondoo  nyingine za tamthilia hii hapa hapa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.