Header Ads

Breaking News
recent

TAMTHILIA YA “MARA CLARA” EPISODE YA 44 KIFO CHA “MARA” SIRI NZITO YA ANZA KUFICHUKA.

CLARA NA MARA

Polisi wanaenda kumkamata Christina, mara anafanikiwa kuwachenga, wakati anatoka nje ya ofisi yake, Gurlly anatokea na gari huku amevaa mask na kumchukua. Gurlly anamficha sehemu, huku akipanga njama za kumkamatisha mauwaji ya “Mara”

Avira amcharukia Amanthe baada ya kuambiwa kuwa Christina ndiye aliyepanga njama za kumuua mwanae, lakini kwa upande wa Clara bado anatumia mwanya huo kuwa na mama yake wa zamani (Avira).

Christian anamuomba mama yake ruhusa na kuamua kwenda mbali kidogo na mji, kule ni kwandugu yake. Kumbe wakati  Christian akiwa mdogo alikuwa anaitwa “Uttoi”. Christian ameamua kuitembelea familia iliyomlea huko kijijini, kumbe Christian ndiye pia aliyemuokota Mara, baada ya bomu kuripuka “Mara” alimpigia simu na kumpeleka huko. Christian amkuta Mara pale kwao kijijini na anajifanya hamjui.Baadae wanakaa pembeni na kukumbukana vizuri.

Huko nyumbani kwa Gurlly maelewano hakuna kwani Clara amemcharukia ile mbaya, kwa mauwaji aliyofanya kwa “Mara”.

Avira atibuana na mama yake Gurlly kwani alienda kumtembelea Clara, mama yake Gurlly hataki kumuona Avira akienda pale, lakini Avira apata nafasi ya kutoka out na Clara.

Christina ampigia simu Amanthe na kumuambia kama atapelekwa jela basi atamripoti polisi kuwa alitumia pesa za kampuni vibaya kwahiyo naye ataenda jela, lakini Avira anasa mazungumzo yao na kuonekana kupunguza jazba kwa mumewe huenda amemsamehe.

Mama yake Gurlly amegundua mchezo wa Gurlly kumficha Christina, kwani amemfuatilia hadi alikomficha na kumuona Christina kwa macho. Sasa bibi huyo aamua kwenda kwa Amanthe na kuonekana kunajambo anataka kumuambia.

Nini kitaendelea, tazama Star TV na karibu tena kwa dondoo  nyingine za tamthilia hii hapa hapa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.