Header Ads

Breaking News
recent

TAMTHILIA YA “MARA CLARA” EPISODE 48 NA 49 – MAJAMBAZI WAZIDI KUIVAMIA NYUMBA YA AMANTE NA MKEWE ALVIRA, WATAKA KITU.


CLARA NA CHRISTIAN (PICHA)
Katika Tamthilia iliyopita Garl anaonekana kuzidisha ukatili dhidi ya Amante, kwani afanikiwa kumtupia kisanga kinachompeleka lumande moja kwa moja.

Christina ampigia simu Amante na kutaka kuueleza ukweli, lakini Gary ashtukia mchongo huo na kumtangulia Amante kufika kwa Christina na kumnyonga hadi kifo. Baada ya Gary kufanya mauwaji hayo anatoroka na kumuacha Amante akiwasili kwa Christina na kumkuta akiwa tayari amekwisha fariki dunia. Akiendelea kushangaa mara polisi wanafika na kumtuhumu kuwa ndiye aliye muua Christina.

Suzan afanikiwa kutoroka na kukutana na MARA watoroka, lakini Gary ashtukia na kuagiza watu wawafuatilie na kuwakamata lakini wanapigwa chenga na basi kuondoka kusiko julikana.

Gury anawatuma majambazi wawili kuvunja nyumbani kwa Alvira ikiwa ni mpango wake wa kufanya Alvira aogope na kumuomba msaada ili ammtie mikononi mwake.

Gary anaanzisha mazoea ya kwenda nyumbani kwa Alvira akijifanya anawapa ulinzi na msaada wowote watakaohitaji. Alvira anamua kupatia kazi ya udereva katika kampuni yao lakini Clara anaonyesha wasiwasi na uamuzi huo.

MARA na Suzan wafanikiwa kupata kazi katika Lordge moja huko walikofikia, pia Alvira amepigiwa simu na Suzan kumueleza kuwa huko waliko wanaendelea vizuri, lakini wakiwa bado wanaongea Clara anafika, Alvira anabaki  mdomo wazi.

Gary anatumiwa Ujumbe wa vitisho nyumbani kwake lakini anamtuhumu Christian kuhusika na vitisho hivyo. Gary anaamua kuuchukuwa Ujumbe ule hadi jela aliko Amante na kumpatia Ujumbe ule akidai kuwa “nakurudishia Ujumbe ulionitumia”. Amante anashangaa na kuukana lakini anacheka na ku muambia Gary kuwa “huenda kuna mtu anajua mkanda mzima wa maovu yako ndo maana anafanya hivi, lakini sitakoma kufuatilia ukweli hadi nihakikishe maovu yako yanafichuka”.

Gary akiwa bado anatafakali ninani anayemfuatilia wakati anafika nyumbani anakuta bahasha na kuifungua. Ndani yake anakutana na picha zake akiwa na majambazi wake huku akiwa ameshikilia bastola. Lakini paia kunawatu wanazidi kumfuatilia na ripoti hiyo imeonekana inapelekwa kwa Alvira.
Alvira anaamua kwenda kumsalimia mama yake Gary, lakini bibi huyo anaonekana kuwa na jambo la kusema. Alvira anampa karatasi na bibi huyo kumuandikia maneno yakiwemo kuhusu pesa na uovu wa Gary. Lakini kwa bahati mbaya Alvira anaisahau karatasi ile chini na Gary kuikuta, anahaha na kuongea kwa ukali akimuuliza mama yake “pesa zangu zikowapi??”

Familia ya Amante akiwemo Yule bibi wa kazi wavamiwa na majambazi tena, lakini pia kwa upande wa Christian yuko hatalini kwani Gary amesema akibaini ndiye anayetuma watu basi utakuwa ndio mwisho wake.

Je nini kitaendelea? Tazama Star TV na karibu tena kwa dondoo  nyingine za Tamthilia hii hapa hapa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.