NDANI YA EPISODE YA 47 YA TAMTHILIA YA "MARA CLARA" - "MARA" AZIDI KUTAFUTWA KILA MAHALI.
Vina saba (DNA) vyaonyesha kuwa waliomzika sio MARA ni
Lenita, lakini bado hali ni tete kwani Garl anadai akimuona MARA atampoteza kwa
mikono yake mwenyewe.
Christian afanikiwa kumuhamishia MARA katika nyumba
nyingine, lakini Garl apata mchongo kutoka wa Clara kuwa huenda Christian akawa
anajua sehemu MARA alipo. Garl anamfuatilia Christiani hadi nyumba alipomficha
MARA, lakini Garl anashindwa kung’amua siri hiyo na kuamua kumtumia mtu
mwingine ili aendelee kuchunguza nyumba hiyo. Jambazi huyo akiwa nje ya nyumba
alimo MARA ikiwa ni mida flani ya usiku, ghafla Christian anajitokeza na bonge
la camera na kumpiga picha Yule jambazi.
Baada ya familia ya Amante kupata uhakika kuwa motto wao
Mara bado yuko hai, waliamua kuchapisha picha za MARA na kuzisambaza kwa kila
mtu ili kubaini alipo MARA. Wakiwa katika zoezi hilo walifika katika duka moja
la mama mmoja ambaye kwa mara ya kwanza MARA aliponusulika kwa bomu alifika
pale na kumuomba apige simu huku sehemu ya uso wake ukiwa unavuja damu – mama Yule
aliwapa Ujumbe huu wazazi wa MARA (Amante na Alvira).
MARA azidi kumtembelea bibi yake kwa siri, japokuwa bibi
huyo anamengi ya kumuambia lakini anashindwa kwa sababu ya ugonjwa wa kupooza
alionao. Bibi huyo ndiye aliyeficha pesa za Garl na kuzichimbia chini ya ardhi
akisema kuwa pesa hizo ni damu ya mjukuu wake MARA iliyomwagika kwaajili ya
pesa hizo.
Amante anaamua kutangaza donge nono la shilingi milioni 10
kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa ya
kumpata MARA. Kumbuka kuwa Clara alihamia kwa “Amante” akitegemea kuwa MARA
hatokuwepo tena lakini mambo yamekwisha badilika, sasa aamua kufanya uchunguzi
wa kuweza kubaini ukweli kama kweli Christian anamficha MARA? Clara anawasili
kwao Christian na kumkuta mama yake Christian, wakati mama huyo akimuandalia
chakula, mara Clara anaamua kufungua begi la Christian na kukutana na picha alizompiga
MARA za hivi karibuni, lakini katika kitendo cha kumaliza kuirudisha camera,
Christian anambamba.
Jambazi wa Garl aliyeko jela anampigia simu Garl na
kumuuliza kuhusiana na ahadi aliyokuwa amemwahidi kuipatia fedha familia yake
ili asitoboe siri kwa polisi, mbona hakuitimiza? Asipofanya hivyo kwa muda
mfupi basi atatoboa ukweli, kwani Amante amemwahidi kumpatia milioni 10.
Garl anachukua uamuzi wa kumtuma mwanamke mmoja ambaye
alijifanya rafiki ya mke wa jambazi aliyeko jera na kumtuma ammpelekee chakula
chenye sumu. Jambazi anafanikiwa kukila chakula kile, ghafla anaanza kutapika
kile chakula.
Garl anampigia simu Clara aondoke mara moja pamoja na Alvira
katika nyumba yao. Clara anajifanya mgonjwa usiku huo, inabidi Alvira ampeleke
hospitali usiku huo. Kumbe Garl anawatuma watu na kuiripua nyumba ya Amante.
Je nini kitaendelea?. Tazama Star TV na karibu tena kwa
dondoo nyingine za tamthilia hii hapa
hapa.

No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA