Header Ads

Breaking News
recent

2 FACE IDIBIA AWAOMBA MSAMAHA MASHABIKI WAKE KWA KUFANYIA HARUSI DUBAI.

Staa wa wimbo wa "African Queen" maarufu kama  2Face Idibia kutoka pande za Nigeria ameonekana kuomba msamaha mashabiki wake baada ya shabiki mmoja wa kike kumchana kwa kutopendezwa na kitendo cha msanii huyo kufungia ndoa yake huko Dubai.

Msanii 2 Face aliamua kufunguka kitu kilichosababisha yeye na mkewe kufunga harusi huko Dubai... hivi ndiyo alivyofunguka hapa chini :-

"Mashabiki wangu, ninaomba msamaha wa dhati kwa sehemu niliyofanyia harusi. I will make it up to you guys. Sababu kuu iliyonifanya nifungie harusi yangu Dubai, ni kwasababu kama ningefungia harusi Nigeria, Mchungaji angeuliza swali kuwa kuna mtu yeyote mwenyepingamizi na harusi hii?

2 Face aliendelea kufunguka - Pia kuna mtu yeyote anayedai kuwa huyu ni mume wake? Na kama ingekuwa hivyo basi mama watoto wangu wote wangesimama na kuweka vipingamizi, hivyo wangeharibu ndoa yangu.
Kwahiyo niliamua kuiweka mbali kwasababu wasingeweza kumudu gharama za usafiri hadi Dubai, na hata kama Mchungaji angeuliza maswali yale, basi ilikuwa ni kiarabu, hakuna mtu ambae angeng'amua tendo hilo" - Hayo ni maneno ya msanii 2Face Idibia.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.