Header Ads

Breaking News
recent

VIDEO YA MAZIKO YA PADRE 'EVARIST MUSHI' HUKO ZANZIBAR.



Ibada maalum ya kumuombea Padre Evarist Mushi imefanyika leo Zanzibar kwenye kanisa katoliki la St. Joseph la Minara miwili na kuongozwa na Askofu mkuu Muadhama Polycarp Cardinal Pengo na kuhudhuriwa na mamia ya waumini wa kanisa hilo.

Wengine waliohudhuria ni viongozi mbalimbali wa kiserekali wakiongozwa na Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein ambapo baada ya ibada safari ya kuelekea Kitope kwenye maziko ilianza kwa msafara wa magari mengi kupita mitaani huku ukiongozwa na gari la Polisi.

Padri Evarist Mushi wa Kanisa katoliki la St Joseph la Minara Miwili aliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akielekea kwenye ibada ya jumapili ya Kanisa la St. Theresia lililoko Mtoni.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.