Header Ads

Breaking News
recent

NJIA RAHISI ZA KUACHA KUVUTA SIGARA

Uvutaji wa sigara ni swala la kisaikolojia linaloweza kuathiri afya ya mwili wako kwa kufanya mazoea ya kuvuta sigara mara kwa mara.

Kuna imani na mazoea yaliyojengeka kwa watumiaji wa sigara kuwa, sigara hukuliwaza na kukuongezea hali mpya ya kuweza ya kufikiria jambo kwa haraka  bila kuumiza kichwa.

Njia zitakazoweza kukufanya uachane kabisa na uvutaji wa sigara.

Hapa lazima uweke mikakati ya kuacha kuvuta sigara, lazima ujue vitu vinavyokusababisha uvute sigara mara kwa mara. Ziandike sababu zoote zinazokufanya uache sigara, tengeneza kopi ya maeelezo hayo, yaweke sehemu zote unapopenda kutunza paketi ya sigara, mfano katika mfuko wa shati, koti, gari ndani ya nyumba nk. Sababu mojawapo za wewe kuacha kuvuta sigara zinaweza kuwe mojawapo kati ya hizi;
  • Nikiacha kuvuta sigara, nitajisikia mwenye afya njema na kuwa na nguvu zaidi, meno meupe na mwenye kupumua vyema.
  • Nitapunguza uwezekano wa kupata ugonjwa wa kansa, ugonjwa wa moyo, kufa mapema na kuwa na makunyanzi ya ngozi kama mtu aliyezeeka.
  • Nitawafanya wa ndugu, jamaa, mpenzi na familia yangu kujivunia kuwa na mtu asiyetumia sigara.
  • Sitawaweka hatarini watoto wangu na watu wengine tena, wakati nitakapokuwa nimeacha kuvuta sigara.
  • Nitapata watoto wenye afya (wewe au mpenzi wako wakati  akiwa mja mzito).
  • Nitatunza pesa nyingi za matumizi badala ya kununua pakti za sigara kila mara.
  • Sitakuwa na shaka tena la kurudia kuvuta sigara.
Njia pekee zitakazokusaidi kuacha kuvuta sigara  endapo utazizingatia kikamilifu na kujitambua kwanza.
  • Panga tarehe maalum ya kuacha kuvuta sigara.
  • Waambie marafiki zako, familia yako na wafanyakazi wenzio kuhusu mpango wako wa kuacha kuvuta sigara.
  • Zifahamu changamoto utakazozipata wakati utakapokuwa umeacha kuvuta sigara, kwa mfano kiu ya kuvuta, unyonge na mengineyo, zitakusaidia kuweza kuzishinda.
  • Ondoa tumbaku na sigara zote katika maeneo yote uzitunziapo kwa mfano nyumbani kazini na hata kwenye gari.
  • Zaidi zungumza na daktari akusaidie kiushauri jinsi ya kuacha kuvuta au kutumia sigara na tumbaku.
Baada ya kuacha kutumia sigara, utakutana na changamoto nyingi ndogo ndogo kama vile, maumivu ya kichwa, uchovu wa mwili, kichwa kuuma, hamu ya kuvuta na hata pia washirika wako watakupa ofa mara kibao za kukununulia sigara. Kamwe usirudi nyuma, songa mbele na msimamo wako kwani mpaka kufikia hapo utakuwa umejiondoa kabishaa na uvutaji sigara na utakuwa na afya njema.

JITAMBUE KWANZA

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.