AIRTEL TANZANIA: WATEJA WAKE KUONGEA KWA SENTI 10 TU KWA SEKUNDE BAADA YA DAKIKA YA PILI.
![]() |
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, akifafanua jambo
jinsi wateja wa Airtel watakavyofaidika na huduma ya punguzo la gharama za
maongezi hadi senti 10 kwa sekunde.
|
Airtel yapunguza gharama za kupiga simu hadi senti 10 kwa
sekunde
* Wateja
kufurahia punguzo la asilimia 70 kupiga simu Airtel kwenda Airtel
* Wateja wa
Airtel kupiga simu kwa senti 10 tu kwa sekunde baada ya dakika mbili
* Hakuna
kujiunga, kila mteja wa malipo kabla ameunganishwa kufurahia viwango hivyo.
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeendelea na dhamira
yake ya kutoa mawasiliano nafuu nchini kwa kutangaza punguzo la gharama za
kupiga simu kwa lengo la kutoa fulsa zaidi kwa wateja wa Airtel wa malipo ya
kabla kuendelea kufurahia huduma za Airtel.
Sasa wateja wa Airtel watatozwa senti 10 kwa sekunde baada
ya dakika ya pili ya maongezi kwa kupiga simu Airtel kwa Airtel.
Akiongea wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo, Mkurugenzi
wa Airtel Bw Sam Ellangallor alisema" tumepunguza gharama zetu za kupiga
simu kwa asilimia 70 ili kuendelela kutoa huduma za kisasa, rahis na za bei nafuu kuweza kukidhi mahitaji ya
wateja wetu sasa kupiga simu Airtel
kwenda Airtel ni kwa bei nafuu zaidi
ambapo wateja wa Airtel watatozwa senti 10 kwa sekundi baada ya dakika mbili za
awali pale watakapopiga simu Airtel kwenda Airtel. Hakuna sababu ya kushindwa
kuwasiliana kwani Airtel inakuwezesha kuongea na familia na marafiki zako siku
nzima bila kikomo kwa gharama nafuu ya senti 10 kwa sekunde"
"Tunafahamu huduma ya mawasiliano ni nyenzo kubwa
kwenye shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wateja wetu, Hivyo ndio maana Airtel
tunajitahidi sana kuwaletea wateja huduma zenye ubunifu wa hali ya juu ili
kutoa unafuu wa mawasiliano zaidi.
Airtel bado tunaendlelea na mkakati wetu wa kupunguza
gharama za mawasiliano ili kutimiza dhamira yetu ya kutoa huduma
bora".aliongeza Elangallor.
Airtel hivi karibuni imepunguza gharama za kutuma sms kwa
kupitia huduma yake ya SMS Kichizi ambapo ujumbe mfupi wa maneno kwenda mtandao
wowote unatozwa shilingi moja mara baada ya kutuma ujumbe mfupi wa kwanza kwa
shilingi 125 tu.
Akitoa maelezo zaidi ya huduma hiyo ya punguzo la gharama
za mawasiliano Mkurugenzi wa mawasiliano
wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya "leo tumewawezesha wateja wake
kuongea kwa senti 10 tu kwa sekundu na kutoa uhuru zaidi wa kuongea.Hakuna haja
kwa mteja wa Airtel kujiunga na gharama hizi mpya nafuu, ukiwa unatumia Airtel
tu moja kwa moja utakuwa umeunganishwa na huduma hii nafuu.
Akizungumza juu ya muda Mallya aliongeza hizi ni gharma za
kudumu zitakazopatikana nchi nzima
Airtel Tanzania ni kampuni inayoongoza kwa kutoa huduma bora
na nafuu kama Airtel money na huduma ya internet ya kasi ya 3.75G. Mwanzoni mwa
mwaka huu Airtel imetoa punguzo la
gharama za ujumbe mfupi (SMS) ijulikanayo kama
SMS kichizi inayowawezesha wateja wakel kutuma kila SMS kwa shilingi 1
kwa siku.
Source: Global Publishers
Source: Global Publishers

No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA