Header Ads

Breaking News
recent

MTANGAZAJI WA TIMES RADIO "DIDA" ALIA NA USHURU, AINGIZE RANGE ROVER KUTOKA MAREKANI.

Asili Yetu Tanzania.Copyright

 
HADIJA Shaibu ‘Dida’ ni mtangazaji the big name Bongo anaye-host program ya Mitikisiko ya Pwani kunako kituo namba moja cha Radio Times FM cha jijini Dar, ambaye amelia na serikali impunguzie ushuru ili aingize nchini gari la bei mbaya aina ya Range Rover kutoka pande za Marekani.
Hot 2 Hot kupitia blog ya presenta huyo imeinyaka kuwa bidada huyo anatamani kuingiza mkoko huo Bongo lakini hofu yake ni juu ya ushuru unaotozwa na Mamlaka ya Mapato (TRA) bandarini, hivyo kuomba kupunguziwa ili naye asukume ndinga hiyo ya bei chafu mjini.
“Jamani TRA nipunguzieni ushuru,” aliandika Dida kwenye mtandao huo wakati amepozi na gari hilo hivi karibuni akiwa likizo huko New York, Marekani.
Dida anatarajiwa kushuka nchini mahususi kwa kuongoza shoo kubwa ya Mitikisiko ya Pwani itakayozikutanisha bendi zote za Taarab zinazotamba Bongo ndani ya kiwanja cha maraha cha Dar Live, Mbagala-Zakhem, Novemba 3, mwaka huu.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.