MAONYESHO YA SANAA YA VITU VYA ASILI YA 'SOBER HOUSE' ALLIANCE FRANCAISE YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.
Asili Yetu Tanzania.Copyright
Kamishna kutoka Tume ya Kuratibu na kudhibiti dawa za
Kulevya nchini Bw. Christopher Shekiondo akizindua rasmi maonyesho ya sanaa ya
Sober House jijini Dar amesema kwa niaba ya tume ya kudhibiti dawa hizo
Zanzibar na kwa Serikali kwa ujumla wanatambua mchango wa wadau mbalimbali
uliosaidia vijana kuachana na tabia hiyo na kuahidi kushirikiana nao katika
kuhakukikisha asilimia kubwa ya vijana wanabadilika kwa kutumia njia mbalimbali
ikiwemo sera madhubuti za Serikali na mipango mikakati ikiwemo utekelezaji wa
Kampeni za ufahamu wa madhara ya madawa hayo.
Ameongeza kusema kuwa mikakati ya kupambana na matumizi ya
dawa za kulevya inakabiliana na changamoto nyingi kutokana na uhaba wa vituo na
wataalamu lakini Serikali haijakata tamaa na inaahidi kutimiza lengo hilo
katika muda muafaka ikishirikiana na wadau mbalimbali na kuomba wadau wengine
wajitokeze.
Mkurugenzi wa Chama cha maafisa Ustawi wa Jamii Bi. Anna
Swai akionyesha Sanamu ya Msanii Mkongwe nchini Bi. Kidude iliyotengenezwa na
mmoja wa vijana waliobadili muelekeo na kuamua kuachana na dawa za kulevya
Zakaria Mwiru (kushoto) wakati wa ufunguzi wa kazi za sanaa.
Mgeni rasmi katika maonyesho ya Sanaa ya 'Sober House'
yaliyozinduliwa jijini Dar es Salaam Kamishna wa Tume ya Kudhibiti Dawa za
Kulevya visiwani Zanzibar Dkt. Shekiondo (wa pili kushoto) katika picha ya
pamoja na wadau wanaondesha mkakati wa kuwasaidia vijana kubadili tabia na
kuachana na matumizi ya dawa za kulevya na badala yale kuonyesha vipaji walivyo
navyo katika sanaa.
Mbunifu
wa Mavazi nchini na Mwenyekiti wa Tanzania Mitindo House (TMH) Khadija
Mwanamboka a.k.a Kubwa la Maadui alikuwa ni miongoni mwa wageni
waliohudhuria uzinduzi wa maonyesho hayo.Pichani akipozi na moja ya
mkoba uliosukwa na mkeka ikiwa ni kazi za vijana waliokuwa wakitumia
madawa ya kulevya na kujifunza fani mbalimbali na mwishowe kuvionyesha
kwa jamii.









No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA