AJALI YA BASI LILOKUWA LIMEBEBA WAJUMBE WA CCM MKOANI MWANZA, YAUWA.
Asili Yetu Tanzania.Copyright
![]() |
| Wananchi wakishangaa ajali ya basi jinsi ilivyotokea. |
BASI lililobeba wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM kutoka wilaya
ya Kwimba limepata ajali na kuanguka eneo la Buhongwa wilaya ya Nyamagana,
mkoani Mwanza majira ya saa 3:30 - 4:00 asubuhi leo.
Imeelezwa kuwa dereva wa chombo hicho cha usafiri amefariki
dunia papo hapo na wajumbe wengine saba kujeruhiwa vibaya na kukimbizwa
hospitali ya rufaa Bugando.
Chanzo cha ajali hiyo kinatajwa kuwa basi hilo lililokuwa
katika mwendo kasi lilikuwa katika harakati za kulikwepa lori aina ya Fusso
ambalo lilikuwa likigeuza kujiweka sawa kuingia barabarani ndipo basi hilo
lilipopoteza uelekeo na kulibamiza Fusso na kupinduka.
Wajumbe hao kutoka wilaya ya Kwimba, walikuwa wakiingia
jijini Mwanza kwenye uchaguzi wa viongozi na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM
mkoa wa Mwanza unaofanyika leo uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.


No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA