Header Ads

Breaking News
recent

'MAMA INSURANCE' MOVIE MPYA KUTOKA NIGERIA ITAKAYO DONDOKA SOKONI SIKU CHACHE.

All rights reserved to Asili Yetu.


 Mama Insurance ni movie mpya ya muigizaji wa kike kutoka Nollywood Nigeria anayekwenda kwa jina la Liz Da Silva.Movie hii imeigiziwa katika kisiwa cha Victoria nchini Nigeria chini ya director Bayo Tijani.

Movie hii imezungumzia mwanamke ambae ni mmiriki wa nyumba (Ayo Mogaji) ambae anawapangaji wa kike pekee.Mwanamke huyo anaelimu ya kutosha na ni mwanamke anayejua umuhimu wa bima.Anawapangaji wa kike -- mmoja ni mfanyakazi wa benki (Fathia Balogun), muongo (Liz Da Silva), Malaya (Ronke Odusanya), na mlokole (Iyabo Ojo). Pia alikuwa na mfanyakazi wa ndani (Shola Williams) na mlinzi (Ronke Ojo).  Mwanamke huyo anamuonyesha upendo wa dhati momoja wa wapangaji wake, bila ya mpangaji huyo kujua mama huyo ni mnafki na muongo.

Liz Da Silva ambaye ndio mwenye movie hii, amesema amefarijika sana kufanya movie hii, kwasababu yeye hupenda kufanya vitu tofauti kabisa na wenzake.Liz amesema movie hiyo ya Mama Insurance itadondoka muda sokoni siku chache.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.