Header Ads

Breaking News
recent

VYUO VIKUU AFRICA HAVITAMBULIWI

Chuo kikuu cha Khartoum
Kuorodhesha vyuo vikuu kulingana na umaarufu ni desturi inayokua kwa kasi sana katika sekta ya elimu ya juu.
Orodha hiyo, inayojumuisha vyuo vikuu vilivyo maarufu zaidi duniani, ina walakini kwani bara zima halimo.
Hutapata hata chuo kimoja kutoka bara la Afrika kwenye orodha hiyo.
Vyuo vikuu vilivyoorodheshwa ni vya Marekani, Ulaya na baadhi kutoka China na Korea Kusini huku Afrika ikiwa imesahaulika.
Mazungumzo yanayohusu utandawazi wa vyuo vikuu yanatumia lugha ya kuvutia iliyorembwa kwa mada ya ushirikiano wa kimataifa, pamoja na mzunguko wa fedha katika mitandao ya kimataifa.
Ni rahisi sana kupotoshwa na mafanikio ya vyuo hivi ambavyo mazoea ni kuwatunukia watu tuzo na kujionyesha.
Swali ni, ikiwa ushindani wa kimataifa wa vyuo hivi utajikita katika hadhi na uwezo wa vyuo vichache, na hivyo basi bara zima likasahaulika, mambo yatakuwa vipi?

Idadi yaongezeka

Kwa mujibu wa taasisi ya takwimu ya shirika la elimu, sayansi, na utamaduni la Umoja wa Mataifa, kuna wanafunzi milioni 4.5 kusini mwa jangwa la Sahara.
Kulingana na orodha hiyo, wanafunzi hawa kutoka bara la Afrika ni kama hawapo.
Bw Thandika Mkandawire
Lakini idadi hii inawakilisha kuwepo kwa ongezeko kubwa. Mwaka 1970, idadi ya wanafunzi Ilikuwa 200,000 katika eneo hilo la Afrika na sasa idadi ya vijana wanaojiunga na chuo kikuu imeongezeka kutoka aslimia moja hadi sita.
Katika takwimu hizi kuna tofauti kubwa zinazojitokeza. Nchini Malawi, takriban asilimia 0.5 ya vijana watajiunga na chuo kikuu wakati Cameroon kiwango kimefikia asilimia tisa.
Pia kuna mienendo tofauti kwa wale wanaoamua kusomea ng'ambo.
Wanafunzi wanaotoka kusini mwa jangwa la Sahara wengi wao husomea nchi za Afrika Kusini na Ufaransa.
Pia wanafunzi kutoka Afrika Kaskazini huenda kusomea Ufaransa.
Tatizo lingine ni kwamba wanawake kutoka bara la Afrika huwa hawajiungi na chuo kikuu kwa wingi.
Ukilinganisha idadi ya wanawake na wanaume katika vyuo vikuu, idadi ya wanaume ndio kubwa zaidi.
Nchini Chad - nchi iliyo kubwa zaidi kushinda nchi za Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zikijumuishwa pamoja - asilimia 0.6 pekee ya wanawake ndio wanaojiunga na chuo kikuu.
Ingawa idadi ya wanafunzi kuongezeka barani Afrika ni jambo zuri, hii itaathiri mambo mengine pia.
Kwa mujibu wa Benki Kuu ya Dunia, ongezeko la idadi ya wanaojiunga na chuo kikuu imeongezeka mno hata kuzidi uwezo wa kifedha wa vyuo hivyo kuajiri wafanyakazi na kununua vifaa.

Mwelekeo tofauti wa ufadhili

Profesa Thandika Mkandawire, mkufunzi wa maendeleo barani Afrika 'African Development' katika chuo kikuu cha LSE alisema, vyuo vikuu vya Afrika bado vinajaribu kurudi katika hali yake kutokana na kukosa ufadhili miaka ya 80 baada ya fedha hizo kuhamishwa kwenye shule za msingi.
Katika enzi za baada ya ukoloni kwenye miaka ya 60 na 70, vyuo vikuu vingi viliibuka barani Afrika lakini hali hii ilisitishwa ghafla. Na wakati maeneo mengine duniani yalikuwa yakiwekeza kwenye elimu ya juu, bara la Afrika lilikosa fursa hiyo.
Profesa Mkandawire alisema "Ukishaangamiza chuo kikuu, ustawishaji wa chuo hicho tena utakuwa si rahisi."
Waandamanaji wadai uwekezaji kwenye elimu
Huenda itakuwa vigumu sana kujaribu kukaribia vipimo vya maendeleo vilivyoko katika vyuo vikuu vingine duniani baada ya 'miaka mingi' iliyopotezwa.
Prof Mkandawire alisema, watu wenye kipato cha kawaida wanajitahidi kushinikiza kuwepo kwa vyuo bora zaidi ili ijadiliwe kwenye duru za kisiasa.
Pia kuna ufahamu kuwa vyuo vikuu ni sekta mojawapo iliyo muhimu katika kuujenga uchumi wa kisasa.
Jo Beall, makamu mkuu wa chuo kikuu cha Cape Town Afrika Kusini (chuo pekee kutoka Afrika kuwa miongoni mwa vyuo vikuu 200 vilivyo bora) alisema "Vyuo vikuu ndio pahala panapo fursa ya kujipandisha katika tabaka za kijamii."

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.