Header Ads

Breaking News
recent

KUUWAWA KWA OSAMA BIN LADEN.

NEWYORK
Barack Obama  

Anti-government protestors watch a TV broadcasting ...
Watu walikusanyika kuangalia tukio kwenye TV
Anti-government protestors watch a TV broadcasting ... 

Pakistani soldiers patrol in the vicinity of ...
Majeshi kuelekea alikokuwa Osama

Osama bin Laden
Osama Bin Laden
 

Kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeda OSAMA BIN LADEN, ameuwawa kilomita 50 kutoka katika mji mkuu wa Pakstan siku ya jumapili ya tarehe 1.5.2011 na mwili wake umepelekwa marekani.

 Rais wa Marekani Barack Obama amethibitisha kuuwawa kwa kiongozi huyo ambaye amekuwa akitafutwa kwa kipindi kirefu sasa.Obama amesema kuwa kikosi cha oparetion hiyo kiliweza kumshambulia kiongozi huyo wa Al Qaeda Osama Bin Laden kwa kushirikiana na urinzi wa sirikali ya Pakistani ambao ndio waliongoza kikosi cha marekani kufika  Abottabad kama kilimita 50 sawa na miles 30 kutoka kusini mwa mji wa Islamabad.

Mbali na mlipuko wa World Trade Centre, kiongozi huyo wa kikundi cha ugaidi alilipua ubarozi wa marekani  Tanzania na kenya mwaka 1998 na 2000 kule Yemen.
Baada ya kutangazwa rasmi kwa taarifa hiyo na Rais Obama, watu walianza kukusanyika nje ya ikulu ya Marekani na kuanza kusherehekea tukio hilo ambalo Rais mstaafu wa marekani George W. Bush amesema ni kitendo cha ushujaa.

Katika tukio hilo la kumkamata kiongozi huyo wa Al Qaeda OSAMA BIN LADEN Rais Obama amethibitisha kutokuathirika na kitu chochota kwa wanajeshi wake huko Pakistani.
Mpenzi msomaji, fungua blog hii tena kwa habari za kina kuhusiana na Mauaji ya Kiongozi huyu wa Al Qaeda.


No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.