Header Ads

Breaking News
recent

JINSI YA KUKABILIANA NA MAISHA MAGUMU.

Karibu mpendwa msomaji katika ukurasa mwingine wa "Ndoto Yetu".Ukurasa unaokupa njia ya kukabiliana na changamoto za hapa na pale zinazokukabili katika maisha yako ya kila siku. Fanya kama  unaangalia hapa chini utapata nini kimejili leo, karibu.

Wahenga walisema “penye nia pananjia” hii inaonyesha kwamba ni njinsi gani walio wengi hushindwa kugundua njia ya kuweza kuwafikisha katika ndoto au malengo yao, hivyo kujikuta wakipoteza nia na kushindwa kutimiza ndoto zao.

Kugundua ni jinsi gani  unaweza kufanikisha malengo yako sii vigumu, isipokuwa unatakiwa kuwa na subira katika malengo yako na hapo ndipo utakapo fanikiwa.

Hutakiwi kukata tamaa katika maisha, isipokuwa unatakiwa kuweka akili na mawazo yako yote kwa kile unachokifanya, huku ukijua kuwa niwapi unataka kufika au nini ungehitaji kupata. “If you heed this advice, and keep your goal firmly in mind, you will find that there is away. Keep going until you find a way that works. Even the ways that don’t work will teach you many things.”

Kuna kitu chochote ambacho ulijaribu kufanya maishani mwako lakini kwa muda ufupi  kikaishia njiani?.Kama ulijaribu tena na tena huenda kwa sasa umeona ni kwajinsi gani kitu hicho ulichojaribu tena kukifanya kimeweza kubadilisha maisha yako!

Naam!! Muda haujaisha kujaribu, fanya hivyo sasa, unaweza ukatupilia mbali ndoto au malengo uliyokwisha fanya ukashindwa, jipange na uanze kujaribu upya, kwasababu mazuri yako mbele.

Usiwe na mategemeo ya haraka haraka kuwa ndoto au malengo yako ya kwanza tu kufanikiwa, hata yakiwa mia moja lakini yasipokuwa na mpangilio mzuri hayataweza kutimia kamwe. Ila tafuta njia mbadala itakayoweza kutumika katika lengo au ndoto yako ya kwanza na siyo kubeba malengo yote kwa wakati moja.

Malengo yaliyo makubwa huchukuwa muda mrefu kufanikiwa, hivyo hutakiwa mwenye malengo hayo kuyarudia kwa mara nyingi, nahii hupelekea watu wengi kushindwa kufikia malengo yao, sii kwamba wameshindwa kabisa bali wameacha kujaribu.Wanafikiri kwamba kama jambo fulani halikufanikiwa kwa haraka basi halitofanikiwa kamwe, “sii kweli”.

“I truly believe that there is a way to have everything you want in life” japokuwa sii kila mara tunaweza kufikia malengo kwa haraka kama wengi tupendavyo.Wakati mwingine ni kwasababu kile tunacho kihitaji au kikusudia sii kile tunacho kifanya, hivyo tunahitaji muda wa kufikiri na kuweka sawa maswala yatakayotupatia furaha maishani mwetu.

Je, umesha wahi kuwa na malengo ambayo ulikwisha kata tama ya malengo hayo na siku moja ghafla yakatimilika bila wewe kutegemea? Nimekuuliza hivyo makusudi kwasababu kile tunacho kihitaji hatuko tayari kukipata, hivyo tunahitaji maandalizi hata ya kisaikolojia. “Katika hali ya kawaida ukiwa na malengo yako wapo watu watasema anaota ndoto za Alinacha but always ili kuwa na mafanikio unaambiwa think big,ukiwaza kupata kidogo utapata kidogo lakini kama unawaza kikubwa basi utapata kikubwa”.

Ni kweli maisha wakati mwingine huwa magumu lakini usikate tamaa, kaza buti, safari ya maisha ni ndefu.
 TEMBELEA JITAMBUE KWANZA

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.