Header Ads

Breaking News
recent

Utafiti: Kufuga Mbwa hupunguza vifo vinavyosababishwa na ugonjwa wa moyo.

Utafiti uliofanywa na wanasayansi nchini Sweden unaonesha kuwa watu wanaofuga mbwa hupunguza hatari ya kifo kutokana na magonjwa ya moyo.

Utafiti huo unaonesha kuwa kufuga mpya hupunguza kwa asilimia 36 hatari ya kifo kwa wenye magonjwa ya moyo hususani kwa wanaoishi peke yao.

Kwenye nyumba ambazo huishi watu wengi, mbwa huwa hawana athari hii moja kwa moja lakini huweza pia kupunguza vifo hivyo vya magonjwa ya moyo kwa asilimia 15 tofauti na watu wanaoishi peke yao wakiwa wanafuga mbwa.

Hatahivyo utafiti huu haujaeleza moja kwa moja kwanini mbwa wanaweza kusababisha manufaa haya lakini imeonesha kuwa watu wanaofuga mbwa huishi maisha ya afya zaidi ya wasiofuga mbwa.

PAKUA NYIMBO ZILIZOTOKA WIKI HII>>>DOWNLOAD
SUBSCRIBE YouTube account yetu upate video zaidi.

Kupata Update kibao, like Facebook account yetu.
Twitter Account yetu>>>Asili Yetu Tanzania
  

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.