HOTUBA YA RAIS KIKWETE KATIKA UZINDUZI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA, HATIMAE AWEKA MAMBO WAZI.
Katika
Hotuba yake iliyofuatiliwa na wengi katika historia ya utazamaji wa
televisheni, rais Kikwete ameonyesha kutoegemea upande wowote japo alikiri kuwa
na haki ya kutoa mawazo yake.
Wengi
wamefurahia uthubutu wake wa kutoegemea upande wowote japo kwa mbali sana hisia
zake ziliweza kudhihirika. Amesisitiza “Maridhiano” ndiyo yatakayowapatia
watanzania katiba bora.
Hata
hivyo makofi yaliweza kusikika kwa wingi kila alipoweza kuelezea changamoto za
muundo wa serikali tatu; kitendo kinachoashiria kwamba wanaopenda serikali
mbili pia wapo, japokuwa bila maridhiano hawataweza kupata ‘Absolute Majority”
vivyo hivyo hata wale wafuasi wa serikali tatu nao watahitaji ‘Political
Compromise’
Ndoto ya
watanzania tuliowengi ni kupata Katiba iliyo bora, isiyo na ubaguzi katika pande
zote, isiyo ya maslahi ya kundi flani na inayozingatia hali ya maisha ya
watanzania wote yani wa hali ya juu na hali ya chini pia.
Rais
amekuwa akiwasisitiza wajumbe wa kuunda katiba, kuwa makini katika utendaji wao
bila kujali chama, kabila wala itikadi binafsi katika swala zima la uundaji wa
Katiba mpya. Binafsi nalitakia Bunge maalum la kuunda Katiba "kila
laheri" katika uundaji wa Katiba mpya itakayo tufaa watanzania wote.

No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA